Rais wa
Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ( pichani) ameteuliwa kuwania tuzo la Forbes la mtu mashuhuri
wa mwaka.
Jarida hilo
la biashara limemtambua Rais Magufuli kwa umuhimu wake katika kuimarisha uchumi
wa taifa hilo.
Wengine
walioteuliwa kuwania tuzo hiyo ni pamoja na Benki ya Capitec nchini Afrika
Kusini,Rais wa Mauritania,Mtetezi wa haki za umma nchini Afrika Kusini na Raia
wa Rwanda.
Kama Rais
Magufuli atafanikiwa kushinda tuzo hiyo, basi Tanzania itakuwa imepata tuzo
hiyo kwa mara ya pili mfululizo kwani mwaka jana 2015, mshindi wa tuzo hiyo
alikuwa Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Makampuni ya Mohammed Enterprises
Tanzania Limited (MeTL Group), Mohammed Dewji.
Utaratibu wa
jinsi ya kupiga kura kwa mwaka huu ni kutumia tovuti ya FORBES AFRICA
ambapo baada ya kuingia hapo, unaweza kugusa jina la mtu ambaye unapendekeza
ashinde tuzo na hapo kura itakuwa imehesabiwa.
Na:BBC Swahili.
|
Wednesday, October 26, 2016
Rais Magufuli kuwania Tuzo la Mtu Mashuhuri.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment