Maradhi ya
vichwa vikubwa na migongo wazi kwa watoto yanatibika endapo wazazi watachukua
tahadhali mapema ya kumpeleka mtoto hospitali kwaajili ya matibabu. Dk Hamis
Shaabani daktari bingwa wa upasuaji wa mishipa ya fahamu kutoka Taasisi ya
mifupa(MOI) ameyasema hayo leo wakati wa zoezi la ufungaji upasuaji wa vichwa
vikubwa na migongo wazi katika hospital ya Mkoa wa Kagera.
|
Mkuu wa mkoa
wa Kagera meja jenerali mstaafu Salum
Kijuu akiwashukuru wawakilishi wa kambi tiba ya GSM Foundation ofisini kwake,Dk
Hamis alisema kuwa utafiti uliofanywa na Taasisi ya MOI mwaka 2002 unaonyesha
zaidi ya watoto 4800 huzaliwa kila mwaka wakiwa na maradhi ya vichwa vikubwa na
migongo wazi na kati yao 500 pekee ndiyo wanaoweza kufika hospital na kupatiwa
matibabu.
Akizungumzia
chimbuko la maradhi hayo Dk Hamisi alisema kuwa watoto wenye vichwa vikubwa na
migongo wazi wanaweza kuzaliwa nacho au kupata siku chache baada ya kuzaliwa.
|
No comments:
Post a Comment