Zaidi ya Milioni
200 zimetolewa kwa Kaya masikini sana 7319 zilizomo wilayani Biharamulo mkoani
Kagera,wakati wa ruzuku iliyotolewa na TASAF III kwa awamu ya sita,ikiwa ni
sawa na asilimia 90% za malengo yaliyokusudiwa.
Kiasi hicho kilitolewa kwa Walengwa waliomo kwenye mpango wa kunusuru Kaya masikini sana
unaotekerezwa na Mfuko wa maendeleo ya jamii (TA SAF III) kwa malipo ya
miezi miwili ikiwa ni mwezi wa Mei na Juni mwaka huu,2016.
Mratibu
wa TASAF III wilayani Biharamulo,Bi. Beata Maganga,mbali na fedha hizo kwenda kwa
walengwa,pia kiasi cha shilingi 4,269,954.55/= zimepelekwa kwenye vijiji
husika,ikiwa ni kila asilimia 1.5% inayotakiwa kubaki kwa kila kijiji,lengo
likiwa ni kutoa uwezesho kwa wajumbe wa serikali ya kijiji ambao wanawajibika
katika majukumu ya usimamizi wa fedha za ruzuku wakati wa ugawaji ruzuku kwa
walengwa.
Bi.Maganga amesema
pamoja na mafanikio hayo,kiasi cha shilingi 250,504,000/= ni malipo ya ruzuku
iliyotolewa kwa walengwa husika,walioko kwenye mpango.
Ametaja mafaniko
yaliyopatikana kwa baadhi ya walengwa wa mpango huo tangu ruzuku hiyo ianze
kutolewa Julai / Agosti mwaka jana,2015 ambavyo hadi sasa ni awamu nne,ni kuanzishwa
kwa miradi midogo midogo ambavyo baadhi ya walengwa wamenunua mifugo na kuanza
kufuga mbuzi,nguruwe na kuku huku wengine wakionesha kununua bati moja moja kwa
ajili ya kujenga makazi mapya tofauti na ya makazi yao ya awali ambayo baadhi
yao waliishi kwenye nyumba za nyasi na zilishaanza kuvuja.
Habari kwa hisani ya ITV
|
Saturday, June 25, 2016
TASAF III:-Zaidi ya milioni 200 zimetolewa Kwa kaya Masikini 7319 wilayani Biharamulo.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment