BUNGENI DODOMA:-Watoto wenye Ulemavu na Changamoto zao kwa Wabunge na Mawaziri. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, June 25, 2016

BUNGENI DODOMA:-Watoto wenye Ulemavu na Changamoto zao kwa Wabunge na Mawaziri.

2.Baadhi ya watoto wenye ulemavu wakiwa kwenye picha ya pamoja na waheshimiwa wabunge na mawaziri nje ya Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wakiwa kwenye picha ya pamoja na waheshimiwa wabunge na mawaziri nje ya Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.

Watoto wenye ulemavu wakiwakilishwa na viongozi wa mabaraza ya watoto wenye ulemavu kutoka mikoa mbalimbali Nchini, wamepata nafasi ya kukutana na wabunge ambao ni wajumbe wa kamati ya Katiba na Sheria na kuanika changamoto zao.

Tukio hilo lilichukua nafasi hivi karibuni baada ya watoto hao kwa msaada wa Free Pentecostal Church of Tanzania (FPCT) kupata fursa ya kuhudhuria vikao vya bunge mjini Dodoma kisha baadaye kufanya mkutano ndani ya Ukumbi wa Pius Msekwa uliowajumuisha Walezi wao, Wabunge na Mawaziri.

Wakieleza changamoto zao mbele ya Wabunge hao pamoja na mgeni rasmi ambaye ni Naibu Waziri (Ofisi ya Waziri Mkuu) Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu , Mhe.Abdallah Possi, watoto hao waliweka bayana mambo mbalimbali yanayowapa wakati mgumu katika maisha yao ikiwa ni pamoja na jinsi wasivyopata haki sawa na watoto wengine.
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wakiwa kwenye picha ya pamoja waheshimiwa wabunge na mawaziri nje ya Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wakiwa kwenye picha ya pamoja waheshimiwa wabunge na mawaziri nje ya Ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma.

Akisoma risala akiwawakilisha watoto wenzake, Kaimu Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Wenye Ulemavu Tanzania, Wilfred Wilbert alisema kwanza anawashukuru FPCT kwa namna ambavyo wameweza kuwasaidia kuwaweka pamoja, kutambua na kuzidai haki zao za msingi.

Mabaraza ya watoto wenye ulemevu yametuunganisha na kutupa wakati mzuri wa kujadili pamoja changamoto zinazotukabili katika mikoa yetu, tumekuwa tukipaza sauti zetu na hata wakati mwingine kushirikiana na viongozi mbalimbali kuwaanika wale ambao wamekuwa wakificha watoto walemavu.

“Changamoto tunazopitia zinazokwamisha malengo yetu ni nyingi lakini nipongeze serikali ambayo kwa namna moja ama nyingine kupitia sauti zetu wamekuwa wakifanyia kazi mambo kama vile miundombinu,” alisema mtoto huyo.

Naye Mhazini wa Watoto Wenye Ulemavu Mkoa wa Tabora, Mpaji Nicolaus alipata nafasi ya kueleza changamoto zinazowakumba ikiwa ni pamoja na ukosefu wa fedha za kuendeshea vikao vya mabaraza na kusafirisha watoto kutoka sehemu moja hadi nyingine pamoja na vifaa vya kutunzia dokyuments’....BOFYA HAPA KUENDELEA KUSOMA HABARI HII.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad