Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba kupitia mtandao wa twitter ameweka namba maalum
ambazo zitakuwa hewani kila siku kwa saa 24 kwa ajili ya kupokea taarifa zozote
kutoka kwa raia wema zinazohusu uharifu, ajali, moto na nyingine ambapo baada
ya kupokea taarifa hizo eshi la Polisi litazifanyia kazi mara moja.
Kupiga namba hizo ni bure ambapo
mwananchi hatotozwa kiwango chochote cha pesa na anaruhusiwa kupiga kupitia
mtandao wowote wa simu.
HAPA CHINI NI…’’ Alichokiandika Mwigulu kwenye twitter: “Piga simu namba 111 au 112 kutoa taarifa
jeshi la polisi kuhusu uhalifu wowote,utapata msaada kwa haraka.”
|
No comments:
Post a Comment