Wataalumu wa madini
kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya
barafu kama inavyofahamika.
Tanzania ni miongoni mwa mataifa
machache duniani yaliyojaliwa kuwa na rasilimali na madini mengi.
Na baada ya kugunduliwa
kwa gesi asili huko Mtwara na dhahabu sasa watafiti kutoka Uingereza wamegundua
hifadhi kubwa zaidi Duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania.
Watafiti kutoka chuo
kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalumu wa madini
kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya
barafu kama inavyofahamika.
Ugunduzi huo umefanyika
katika eneo la bonde la ufa la Tanzania.
Katika taarifa kwa
wanahabri huko Japan, watafiti hao wanasema kuwa uhaba wa gesi hiyo kote
duniani ulikuwa umesababisha taharuki haswa kwa madaktari ambao wanatumia gesi
hiyo adimu kuendesha mashine za utabibu zijulikanazo kama MRI scanners, mbali
na kutumika katika mitambo ya kinyuklia miongoni mwa sekta zingine nyingi za
kawi na teknolojia.
Kabla ugunduzi huo
watafiti walikuwa wamebashiri ukosefu wa gesi hiyo baridi ifikapo mwaka wa
2035.
|
No comments:
Post a Comment