Saa chache tu baada ya timu ya
kandanda ya Uingereza kubanduliwa nje ya mashindano ya mwaka huu ya Euro 2016,
Kocha wa Uingereza Roy Hodgson amejiuzulu wadhfa wake.
Hodgson alikuwa
ameshuhudiwa uingereza ikiambulia kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Iceland katika
mkumbo wa 16 bora huko ufaransa.
Kocha huyo mwenye umri
wamiak 68 amekiongoza kikosi hicho cha Uingereza kwa miaka 4 sasa.
Hodgson alichukuwa
wadhfa huo kutoka kwa kocha muitaliano Fabio Capello aliyetimuliwa kufuatia
matokeo duni.
Hata hivyo kocha huyo
hajakuwa na wakati mzuri kileleni mwa Uingereza, Hodgson ameiongoza Uingereza
kushinda mechi tatu tu kati ya 11 alizoshiriki katika michuano mikubwa ya dunia
.
Lakini kitumbua chake
kiliingia mchanga baada ya Iceland - yenye jumla ya watu 330,000 - na moja kati
ya timu za mataifa yaliyoorodheshwa ya chini kabisa katika orodha ya FIFA ya Ubora Duniani kwa Mataifa ya EURO 2016 ikiwa nafasi ya 34,ilipoinyuka Uingereza.
|
No comments:
Post a Comment