Mbunge wa Mbeya Mjini,CHADEMA ,Mhe. Joseph Mbilinyi.
Bunge limeridhia pendekezo la adhabu ya kumsimamisha vikao 10 kuanzia leo,June 30,2016, Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe.Joseph Mbilinyi baada ya kutiwa hatiani na Kamati ya
Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa kudharau mamlaka ya Spika.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Kepten Mstaafu George Mkuchika alisema alinyoosha
kidole cha kati kwenda juu cha mkono wa kulia huku vingine akivikunja jambo
ambalo ni matusi na dharau kwa mamlaka ya Bunge.
Naibu Spika Dk Tulia Ackson amewasimamisha Wabunge wengine wawili wa
UKAWA ,ambao ni Mbunge wa Ubungo (CHADEEMA) Mhe.Saed Kubenea kwa kutohudhuria
vikao vitano kuanzia leo baada ya kutiwa hatiani na Kamati ya Haki, Maadili na
Madaraka ya Bunge kuwa alisema uongo Bungeni.
Mbunge mwingine aliyesimamishwa ni Mbunge wa Simanjiro
(CHADEMA) Mhe.James Ole Millya kutohudhuria vikao vitano kuanzia leo baada ya
kutiwa hatiani na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuwa alisema
uongo Bungeni.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa ameanza kutoa hotuba ya kuahirisha Bunge na
kueleza bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 ni ya kihistoria tangu nchi ipate uhuru kwa kutenga asilimia 40
ya Sh29.5 trilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo.
Kufuatia kuahirishwa
huko, kuanzia kesho Julai Mosi,2016 Serikali itaanza kutekeleza miradi na mpango
mingine iliyoanishwa katika bajeti hiyo.
|
No comments:
Post a Comment