Poland na Ureno leo,
June 30, 2016 wanakutana katika mchezo wa robo fainali ya kwanza kabisa katika
michuano ya Euro mwaka huu, mchezo utakaofanyika kunako dimba la Stade
Vélodrome lililopo jijini Marseille.
William Carvalho, Pepe
na Ricardo Quaresma wote kwa pamoja wana kadi za njano na ikiwa leo
watapata kadi nyingine na timu yao kufuzu hatua ya nusu fainali basi wataukosa
mchezo huo.
Vivyo hivyo kwa upande
wa Poland, Kamil Grosicki, Artur Jedrzejczyk, Krzysztof Maczynski, Michal
Pazdan, Slawomir Peszko, Lukasz Piszczek wote wana kadi za njano.
Takwmu za michezo waliyokutana.
- Hii inakuwa ni mara ya tatu kati
ya Poland na Ureno katika michuano mbalimbali.
- Poland walishinda 1-0 mwaka
1986 katika fainali za Kombe la Dunia na baadaye Ureno kushinda 4-0 katika
fainali za Kombe la Dunia mwaka 2002.
- Poland hawajapoteza dhidi ya
Ureno katika michezo yao mitatu ya mwisho (wameshinda mara moja, wametoka
sare mara mbili).
- Mara ya mwisho kukutana, timu
hizi zilitoka sare ya 0-0, mchezo uliofanyika Warsaw mwaka 2012.
Kuanzia Ijumaa hadi Jumapili kila
Siku itachezwa Mechi moja za Mechi zilizobaki za Robo Fainali.
Wales v Belgium (Ijumaa,Julai 01,2016 Saa 4 Usiku)
Germany v Italy (Jumamosi,Julai 02,2016 Saa 4
Usiku)
France v Iceland (Jumapili,Julai 03,2016 Saa 4
Usiku)
|
No comments:
Post a Comment