Rais wa Tanzania ,Dkt.John
Magufuli amewataka watendaji wote wa Serikali kuhakikisha kuwa wanatekeleza
ipasavyo matakwa ya ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa ndicho kinachoongoza
nchi kwa sasa.
Rais Magufuli
ametoa agizo hilo leo,February 06,2016 kwenye sherehe za miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama cha
Mapinduzi zilizofanyika katika uwanja wa Namfua mjini Singida.
Rais
Magufuli ambaye alikuwa ni miongoni viongozi Wakuu wa Serikali waliohudhuria
sherehe hizo akiambatana na Makamu wake ,Bi.Samiah Suluhu Hassan na Waziri Mkuu,Bw.
Kassim Majaliwa, amesema yeye na serikali yake wamejipanga kutekeleza
kikamilifu ilani ya CCM na kwamba hawezi kukiangusha chama hicho.
Akitoa salaam
zake katika sherehe hizo, Rais Magufuli ametumia muda usiozidi dakika 10 kueleza
mambo ambayo tayari serikali yake imeanza kuyafanya na ambayo itaendelea
kuyafanya ikiwa ni pamoja na "kutumbua majipu" kwa ustawi wa maisha
ya watanzania wote bila kujali vyama vyao.
Ametumia
nafasi hiyo kuwaagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na Watendaji wote
Serikalini kufanya kazi kwa nguvu, Uadilifu na Uzalendo ili kuwaletea
watanzania maendeleo, na kwamba atakayeona hawezi atamuweka pembeni ili wengine
wafanye kazi.
“Nawaeleza
watendaji wote serikalini kuwa atakayeshindwa kufanya kazi, nitamueleza kwa
upole sana maana mimi ni mtu mpole, nitamuambia akae pembeni apishe wengine”
Rais
Magufuli pia ameupongeza uongozi wa CCM mkoa wa Singida kwa kuchangia madawati
1000 kwa shule za Singida na kuwaagiza wakuu wote wa mikoa na wilaya
kuhakikisha wanafunzi hawakai chini.
“Mh
mwenyekiti inasikitisha sana kuona sisi tunajifungia kwenye maofisi makubwa
yenye viyoyozi, na maviti ya kuzunguka lakini tukitoka tu nje tunakuta
wanafunzi wamekaa chini kwenye mavumbi, sasa nawaagiza wakuu wa wilaya na wakuu
wa mikoa hakikisheni wanafunzi hawakai chini”
Rais
Magufuli pia ametumia nafasi hiyo kukishukuru Chama cha Mapinduzi kufanikisha
yeye kuwa Rais kwa kuwa bila chama hicho yeye asingekuwa Rais.
“Nataka
watanzania wote wajue kuwa bila CCM mimi nisingekuwa Rais wao, kwa hiyo huwezi
kunitenganisha mimi na CCM, ndiyo maana leo nimekuja nimevaa kijani yangu hapa”
Pia amesema
haoni kama kuna chama kingine chochote kitakachokuja kutawala Tanzania zaidi ya
CCM
"Nataka
ifikie hatua watanzanie wote wasiwaze wala kuota vyama vingine, tutafanya yale
ambayo wao wanataka kuyafanya, ... Hakuna mtawala anayetaka kutawaliwa, tena
kwa bahati mbaya atawaliwe na vyama vya hovyohovyo, CCM itaendelea
kutawala"
Na:-Mpekuzi
blog.
Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na Mimi Hapa...FACEBOOK .. TWITTER .. INSTAGRAM … Pia Usisite kututumia tukio la Picha/Habari kwa WhatsApp +255789925630/+255756830214.
|
No comments:
Post a Comment