Timu ya
Leicester City, Leo February 06,2016 wameibonda Timu ya Pili Manchester City
Bao 3-1 kwenye Uwanjani wa Etihad Stadium na kupaa kileleni mwa Ligi
wakiwa Pointi 6 mbele.
Magoli
mawili ya Beki Robert Huth na moja la Riyad Mahrez ndizo ziliiua Manchester
City huku Sergio Aguero akiipa City Bao lao pekee.
|
Mbali ya
kuifunga Timu ya 3 ,Tottenham kwao White Hart Lane Mwezi Januari, ushindi huu
wa Leo umeonyesha wazi kuwa sasa Leicester wanao uwezo kuwa Mabingwa wa England
tofauti na dhana ya wengi kuwa watateleza.
Mechi ijayo
kwa Leicester ni huko Emirates hapo Februari 13 dhidi ya Arsenal.
Kwa matokeo
hayo vijana wa Claudio Ranieri wanaendelea kuongoza ligi wakiwa na pointi 53
wakifuatiwa na City ambao wanabaki na pointi zao 47.
|
No comments:
Post a Comment