TAZAMA PICHA:Rais wa Tanzania Dkt.Magufuli alivyokutana na Maalim Seif leo Dec.21,2015 Ikulu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 21, 2015

TAZAMA PICHA:Rais wa Tanzania Dkt.Magufuli alivyokutana na Maalim Seif leo Dec.21,2015 Ikulu.

Bado tunajua Zanzibar hakupatikana Rais mpaka sasa kutokana na mgogoro wa kisiasa unaoendelea..

Kumekuwepo na sintofahamu baada ya Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim kuyafuta matokeo yaliyomtangaza mgombea Maalim Seif kuwa Rais wa Zanzibar hali iliyopelekea mpaka sasa kushindwa kufikia muafaka.

Ujio wa Maalim Seif kwenye Ikulu ya Dar es salaam unakuwa wa pili mara baada ya awali kuja kuonana na Rais mstaafu Jakaya Kikwete, leo Desemba 21,2015 amekutana tena na Rais Magufuli ikiwa ni muendelezo wa mazungumzo yao kuhusu muafaka wa kupatikana kiongozi atayewaongoza wananchi wa visiwa hivyo.

Hizi ndio picha zinazomuonyesha Maalim Seif akiwa Ikulu na kufanya mazungumzo na Rais Magufuli.
maalim

maal2

maal3

maalim4

maalim5
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad