KOMBE LA DUNIA 2018:-Hizi ndo Nchi 20 za hatua ya makundi baada ya Matokeo ya Jana November 17,2015. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, November 18, 2015

KOMBE LA DUNIA 2018:-Hizi ndo Nchi 20 za hatua ya makundi baada ya Matokeo ya Jana November 17,2015.


Kikosi cha timua ya soka ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kilichofungwa mabao 7-0 usiku wa Jana November 17,2015 na wenyeji Algeria mjini Blida katika mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia 2018,kinatarajiwa kuondoka leo November 18,2015 (Jumatano) asubuhi na itafika Dar es Salaam Alfajiri ya Alhamisi.

 Safari ya nchi  20 zitakazoingia hatua ya Makundi ya kuwania Nafasi 5 za Afrika kwenye Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Russia zimekamilika hiyo Jana baada ya Mechi za Marudiano za raundi ya Pili huku Tanzania ikicharazwa 7-0 na Algeria na kutupwa nje.

Tanzania, wakicheza ugenini, walidundwa 3-0 hadi Mapumziko na kwenda hiyo Haftaimu wakiwa pungufu baada ya Mudathir kula Kadi Nyekundu katika Dakika ya 41 baada ya kupewa Kadi za Njano 2 ya kwanza ikiwa katika Dakika ya 1 tu ya mchezo.

Tanzania, ambayo ilitoka 2-2 na Algeria katika Mechi ya Kwanza, ilipewa Jumla ya Kadi za Njano 7 na kufungwa kwa Penati 2 juu yake kwenye Mechi hii iliyochezeshwa na Refa Sidi Alioum kutoka Cameroun.

Tanzania sasa imetupwa nje ya safari ya kwenda Russia kwenye Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa Mwaka 2018 kwa kucharazwa Jumla ya Mabao 9-2 na hizi ni Bao nyingi mno kufungwa kwake Miaka hii ya hivi karibuni.

NCHI 20 ZILIZOFUZU HATUA YA MAKUNDI.
-Gabon
-Zambia
-Uganda
-Congo DR
-Morocco
-Guinea
-Libya
-Cameroun
-Ghana
-Congo
-Nigeria
-Egypt
-Tunisia
-South Africa
-Ivory Coast
-Burkina Faso
-Algeria
-Cape Verde
-Senegal
-Mali

**Timu hizi 20 zitapangwa Makundi Matano ya Timu 4 kila moja na Mshindi wa kila Kundi kutinga kwenye Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Russia.


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad