ELIMU BURE TANZANIA:-Waraka wa Kufuta Ada Elimu ya Sekondari ( Kidato cha 1 Hadi 4) na Michango yote Elimu ya Msingi . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, November 29, 2015

ELIMU BURE TANZANIA:-Waraka wa Kufuta Ada Elimu ya Sekondari ( Kidato cha 1 Hadi 4) na Michango yote Elimu ya Msingi .

Serikali imeamua kutoa elimu pasipo malipo kwa elimumsingi kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha nne,kuanzia mwaka wa masomo wa 2016.

Azima hii ya serikali ni katika kutekeleza sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 ambayo ina lengo la kuhakikisha kwamba watoto wote wa Tanzania wanapata Elimu bila kikwazo ikiwemo ada au malipo.

 Katika kutekeleza maamuzi hayo,ada zote zilizokuwa zikilipwa kwa ajili ya elimu ya kidato cha kwanza hadi cha nne zimefutwa.Pia, waraka wa Elimu namba 8 wa mwaka 2011 kuhusu michango shuleni nao pia umefutwa.

Aidha, mwongozo wa elimumsingi bila malipo unaandaliwa na utatumwa kwa wamiliki wa shule ifikapo au kabla ya tarehe 15 Disemba 2015.

Waraka huu umeanza kutumika tarehe 21 Novemba 2015.


Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad