KAMPENI URAIS UKAWA 2015:-Edward Lowassa aahidi kurahisisha Biashara Mipakani. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, October 08, 2015

KAMPENI URAIS UKAWA 2015:-Edward Lowassa aahidi kurahisisha Biashara Mipakani.

Taswira ya Bango lenye picha ya Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Edward Lowassa, likiwa kwenye mkutano wa kampeni   Namanga, Jimbo la Longido, jana October 7, 2015, uliofanyika kwenye Uwanja wa Namanga, Jijini Arusha .

 Edward Lowassa, akiwahutubia wananchi wa Mji wa Namanga, Jimbo la Longido,amewataka Watanzania  kujifunza kuchangamkia fursa za ajira zinazotolewa na Afrika Mashariki kama ilivyo kwa nchi nyingine.

 Pia Edward Lowassa ameahidi kuboresha huduma za kibiashara katika maeneo ya mipakani ili kurahisisha biashara tofautina ilivyo hivi sasa.

Lowassa alisema iwapo atachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, atahakikisha kuwa watanzania wanachangamkia fursa za Afrika Mashariki kama ilivyo kwa Kenya.

Napenda mahusiano ya Afrika Mashariki yawe ya kweli na siyo upande mmoja unafaidi na mwingine haufaidi,”alisema na kuongeza kuwa:
  
 
Watanzania wakiwa wanapita kwenye mpaka wa Namanga wasisumbuliwe wapite bila shida.”


Hivi ndivyo hali ilivyokuwa kwa vijana wa eneo la Kisongo, walipokuwa wakimsindikiza mpendwa wao.


Sehemu ya wananchi wa eneo la Kisongo, Jijini Arusha wakiwa wamefunga barabara kuzuia msafara wa Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, ili waweze kumsalimia na kumsikiliza, wakati alipokuwa njiani kuelekea eneo la Ngaramtoni mpaka Namanga, kwenye Mkutano wa Kampeni, hapoa jana Oktoba 7, 2015.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI, ARUSHA.





Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad