MBIO ZA UCHAGUZI - AUGUST.04.2015 | AZAM TV:-Magufuli achukua fomu, Kikwete arusha kijembe. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, August 04, 2015

MBIO ZA UCHAGUZI - AUGUST.04.2015 | AZAM TV:-Magufuli achukua fomu, Kikwete arusha kijembe.

Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.John Pombe Magufuli ambaye aliambatana na mgombea mwenza, Samia Suluhu leo Agosti 04,2015 amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo katika ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Baada ya kuwasili katika ofisi hizo, wagombea hao walitumia muda wa dakika 27 kukamilisha zoezi la kuchukua fomu kisha kurejea katika viwanja vya ofisi za CCM makao makuu Lumumba kuungana na Rais Jakaya Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa CCM aliyeongozana na mkewe Salma Kikwete, kuhutubia mamia ya wanachama wa chama hicho waliojitokeza kuwasindikiza wagombea kuchukua fomu.

Akizungumza baada ya kukaribishwa na Kinana, Rais Kikwete alinzakuzungumza huku akivirushia dongo vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwamba wamechukua “makapi ya CCM” huku akisema, “ Wale wanaodhani CCM ni ya mchezo watakiona cha mtema kuni.

Huku akiongeza kuwa watu wenye tama kupitiliza Tumejiandaa vya kutosha na tutashinda. Uwezo tunao, maarifa tunayo tutashinda. Tujipange kwa hoja za kuzungumzia uzuri wa CCM.”

“CCM jiandaeni kushangilia ushindi….Utawala bora upo, demokrasia ipo, uhuru wa habari upo, watu wanajiunga na vyama vya siasa kwa uhuru, uchumi unakuwa na maendeleo yanaendelea kupatikana,” amesema Rais Kikwete.

Magufuli amesema, “leo tumechukua fomu, tutaizungusha kuweza kupata wadhamini. Nimepokea kijiti hiki kwa mikono miwili. Mategemeo ya watanzania ninayajua. Uongozi wa awamu ya nne uliweka msingi mzuri. Nitaipeperusha vizuri CCM kwa maslahi ya watanzania wote bila kujali chama,” amesema Magufuli...........
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Mhe Abdurahman Kinana akizungumza jambo.
Wagombea hao ambao walivuta umati mkubwa wa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, walipitia Barabara  ya Morogoro, Bibi Titi Mohamed na Ohio kuelekea katika ofisi Tume ya taifa ya Uchaguzi -NEC wakitokea Ofisi za CCM, Lumumba ambapo shughuli kadhaa za watu zilisimama kwa ajili ya tukio hilo huku pia wakionekana kivutio na wananchi kusikika wananchi wakiimba nyimbo mbalimbali.
Mgombea Urais wa CCM, John Magufuli akiwa na Mgombea mwenza wake, Samia Suluhu wakionesha fomu ya kuwania Urais.

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad