![]() |
|
Mbunge wa Mkuranga mkoani
Pwani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima akiangushwa kura za
maoni CCM na ambaye alisema kuwa hakuridhishwa na mwenendo mzima wa kura za
maoni kwa vile umechukua siku tatu bila mawakala kusaini fomu za matokeo.
NIPASHE | 5th Aug 15
Mbunge wa Mkuranga mkoani
Pwani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha,
Adam Malima amesema kuwa kura za maoni zilizopigwa jimboni humo hazikuwa
huru na haki kwa madai kwamba waliopiga kura walikuwa wachache lakini kura za
matokeo zikawa nyingi.
Akitangaza matokeo hayo,
Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni
Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Hadija Kusaga, alisema kuwa waliojiandikisha
kupiga kura walikuwa 46,904, kura zilizopigwa ni 26,949 na kwamba kura 904 ziliharibika.
Alisema kuwa katika matokeo
ya kura hizo, mkuu wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, Abdallah Ulega, aliibuka na
ushindi kwa kupata kura 16, 294 huku Malima akipata kura 8, 212. Aliwataja
wagombea wengine kuwa ni Shukuru Ngweshani kura 356, Jafari Ndande kura 479 na
Maulid Zolange Kura 809.
NIPASHE | 5th Aug 15
Mbunge wa Jimbo la Ubungo,
John Mnyika (Chadema), ameshinda katika kura za maoni za kugombea ubunge katika
Jimbo la Kibamba kwa kupata kura 65 kati
ya kura 80 zilizopigwa (asilimia 65).
NIPASHE | 5th Aug 15
Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo,
Samson Mwigamba , amechukua fomu ya kugombea ubunge katika Jimbo la Ubungo
ambako atapambana na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi wa tiketi ya
Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Said Kubenea wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema).
HABARI LEO | 5th Aug 15.
Mbunge wa Viti
Maalumu Chadema, Chiku Abwao ndiye atakayepeperusha bendera ya
ACT kuwania ubunge wa Jimbo la Iringa mjini katika uchaguzi mkuu ujao, huku
akitamba kwamba atambwaga mbunge anayemaliza muda wake, Mchungaji Peter Msigwa
(Chadema).
Mbali na Abwao
aliyejiunga na ACT Wazalendo hivi karibuni, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa
Chadema, Abuu Changawa naye ameiacha Chadema na kujiunga
ACT Wazalendo, huku akitangaza kuwania udiwani katika Kata ya Mivinjeni, mjini
hapa.
Abwao aliyewahi
kuwa mbunge wa NCCRMageuzi, alisema; “Nimeondoka
Chadema baada ya kubanwa kila kona na Mchungaji Msigwa akidhani kwamba mimi
nilikuwa Chadema kwa sababu ya kutaka cheo.”
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Wednesday, August 05, 2015
Home
SIASA
MBIO ZA UBUNGE 2015:-Fahamu kuchugua fomu kwa Migamba ACT, Mbunge Mnyika na Adam Malima kutoridhishwa na kura za maoni CCM.
MBIO ZA UBUNGE 2015:-Fahamu kuchugua fomu kwa Migamba ACT, Mbunge Mnyika na Adam Malima kutoridhishwa na kura za maoni CCM.
Tags
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Labels:
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment