|
Leo Al
hamisi ya August 06, 2015 ambapo
Mwenyekiti wa C.U.F Prof. Ibrahim Lipumba kakutana na Waandishi wa habari Dar
es salaam kutangaza maamuzi yake magumu siku chache baada ya Edward Lowassa
kujiunga na UKAWA.
Tamko hilo
la Prof. Lipumba linahitimisha siku mbili za minong’ono na tetesi zilizogubika
medani ya kisiasa nchini kuwa kiongozi huyo anaondoka katika chama hicho hali
iliyolazimu wananchama, wapenzi na mashabiki wa kiongozi huyo kufurika makao
makuu ya chama hicho Buguruni Dar es Salaam jana ili kujua hatma ya kiongozi
wao huyo.
Akizungumzia
sababu za kujiuzulu kwake, Profesa Lipumba amesema amekerwa na hatua ya Umoja
wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambao CUF ni chama shiriki kushindwa kusimamia
makubaliano yaliyopelekea kuundwa kwa umoja huo.
Amesema
Ukawa ulianzishwa kulinda maslahi ya wananchi yaliyoainishwa kwenye Katiba
iliyowasilishwa kwenye Bunge Maalumu la Katiba, na kwamba nafsi yake inamsuta
hivi sasa kuendelea na uongozi huku waliokuwa wanaipinga Rasimu ya Katiba ya
Jaji Warioba wakikaribishwa kuwania uongozi wa nchi kupitia umoja huo.
Prof.
Lipumba amesema baada ya kujiuzulu atajikita kufanya shughuli za kitaaluma kwa
kujihusisha zaidi na ushauri wa masuala ya uchumi na maendeleo.
SIKILIZA
/TAZAMA VIDEO YA MKUTANO WAKE HAPA CHINI.
|
No comments:
Post a Comment