Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa pamoja na Mgombea
mwenza, Mh. Juma Duni Haji wakiwasili kwenye viwanja vya Jangwani Jijini Dar es
salaam, kulikofanyika Mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za Chama hicho, Agosti 29,
2015.BOFYA HAPA KUISOMA HOTUBA YA Mh.LOWASSA.
PICHA ZOTE
NA OTHMAN MICHUZI.
Hii leo August 30,2015, Mh Edward Lowassa akiambatana na
waziri mkuu mstaafu Mh Fredrick Sumaye wameanza kazi ya kunadi sera zao mikoani
katika mkoa wa Iringa huku wakiendelea kuungwa mkono na maelfu ya wananchi na
viongozi akiwemo aliyewahi kuwa waziri katika wizara mbalimbali mh Joseph
Mungai.
Wakiwa
mkoani Iringa kwenye mikutano iliyofanyika Mafinga wilayani Mufindi, Ilula
wilayani kilolo na Iringa mjini wanasiasa hao pamoja na kunadi sera na
kuwaombea kura wagombea wao wa ubunge na udiwani wameendelea kuelezea athari zinazolikabili taifa
zinazochangiwa na usimamizi na ubabe wa viongozi wa CCM na wamewataka
watanzania kuendelea kuunganisha nguvu na kukiondoa madarakani sambamba na kuelezea
azma yake ya dhati ya kufanya marekebisho makubwa na kwa wakati na kuzisimamia
kikamilifu.
|
Umati wa
wakazi wa Jijini Dar es salaam, ukiwa umefurika kwa wingi kwenye viwanja vya
Jangwani kuwalaki Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika
mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh.
Edward Lowassa pamoja na Mgombea mwenza, Mh. Juma Duni Haji, walipokuwa
wakiwasili viwanjani hapo, kulikofanyika Mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za
Chama hicho, Agosti 29, 2015.
|
Wafuasi wa
Vyama vinavyounda UKAWA wakiwashangilia Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA), Mh. Edward Lowassa pamoja na Mgombea mwenza, Mh. Juma Duni Haji,
walipokuwa wakiwasili viwanjani hapo, kulikofanyika Mkutano wa Uzinduzi wa
Kampeni za Chama hicho, Agosti 29, 2015.
|
Wafuasi wa
Vyama vinavyounda UKAWA wakionyesha furaha yao kwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa.
|
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akisalimiana na
Mgombea Urais wa Zanzibar katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi
CUF, Maalim Seif Sharif Hamad wakati alipowasili kwenye viwanja vya Jangwani
Jijini Dar es salaam, kulikofanyika Mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za Chama
hicho, Agosti 29, 2015.
|
Sehemu ya
Wanahabari kutoka Vyombo mbali mbali nchini wakiendelea kuchukua habari za
Mkutano huo, uliofanyika jioni ya Jumamosi kwenye viwanja vya Jangwani Jijini Dar es
salaam na kuhudhulia na maelfu ya Wakazi wa jiji hilo.
|
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe akimkabidhi,
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA
kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa pamoja
na Mgombea mwenza, Mh. Juma Duni Haji, Kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya Chama
hicho kwa mwaka 2015/2020 mara baada ya kuizindua, Jana Agosti 29, 2015.
|
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Mgombea mwenza, Mh.
Juma Duni Haji pamoja na Mgombea Urais wa Zanzibar katika mwamvuli wa UKAWA
kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad wakionyesha vitabu cha
Ilani ya Uchaguzi mara baada ya kuzinduliwa na Mwenyekiti wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe.BOFYA HAPA KUISOMA HOTUBA YA Mh.LOWASSA.
|
Viongozi wa
Vyama mbali mbali vinavyounda UKAWA wakionyesha Ilani hiyo mbele ya maelfu ya
wakazi wa Jiji la Dar es salaam, Agosti 29, 2015.
|
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Freeman Mbowe (kulia)
akiwatambulisha baadhi ya Wagombea Ubunge katika Majimbo mbali mbali ya jijini
Dar es salaam.
|
Mwenyekiti
Mwenza wa UKAWA, Mh. James Mbatia akizungumza kwenye Mkutano huo.
|
Watu wa
Msalaba Mwekundu wakiwa wamembeba mmoja wa wakazi wa Jiji la Dar aliepoteza
fahamu kwa kukosa hewa kutokana na uwingi wa watu uliofurika kwenye viwanja vya
Jangwani, Jijini Dar es salaam Agosti 29, 2015.
|
Waziri Mkuu
Mstaafu, Mh. Fredrick Sumaye akitoa salamu zake kwa wakazi wa Jiji la Dar es
salaam waliofurika kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam Agosti
29, 2015.
|
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akiteta jambo na
Mgombea Mwenza wake, Mh. Juma Duni Haji, wakati wa Mkutano wa Uzinduzi wa
Kampeni za Chama hicho, uliofanyika Agosti 29, 2015.
|
Mgombea
Urais wa Jamhuri ya Muungani wa Tanzania katika mwamvuli wa UKAWA kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akihutubia katika
Mkutano huo wa Uzinduzi wa Kampeni za Chama hicho, uliofanyika Agosti 29,
2015.
|
Mmoja wa
wanasiasa wakongwe waliotoka CCM, Tambwe Hiza akisalimia.
|
No comments:
Post a Comment