Kiongozi
Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto akihutubia katika uzinduzi huo na kusema bila
ya kurejesha miiko ya uongozi haitawezekana kupiga vita rushwa na ufisadi
ambapo amepinga siasa zinazofanywa na baadhi ya vyama vya kutaka kukomesha
ufisadi na rushwa kwa kutumia baadhi ya viongozi waliowasababishia wananchi
shida na kadhia mbalimbali wanazozipata.
|
Mshauri wa
Chama cha ACT-Wazalendo, Profesa Kitila Mkumbo akihutubia kwenye uzinduzi huo.
|
Kiongozi
Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto (kushoto), akiteta jambo na Mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha
ACT-Wazalendo, Anna Mghwira.
|
Viongozi
mbalimbali wa chama hicho wakiimba wimbo wa taifa.
|
Kiongozi
Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto, akiwatambulisha wagombea ubunge
wa majimbo yote ya Dar es Salaam.
|
Kiongozi
Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Kabwe Zitto, akigawa ilani ya chama hicho kwa
mgombea urais na mwenza wake.
|
Mgombea
Mwenza, Hamad Mussa Yusuph akihutubia kwenye uzinduzi huo ambapo mara kukabidhiwa
ilani ya chama cha ACT wazalendo, ameahidi kukomesha kero za watanzania na kuwataka kutumia kura zao katika
kufanya mabadiliko badala ya kutumia nguvu na vurugu kama baadhi ya raia wa
nchni nyingine duniani wanavyofanya.
|
Mwana muziki
Bwana misosi, akitoa burudani katika uzinduzi wa kampeni wa Chama cha
ACT-Wazalendo uliofanyika viwanja vya Zakhem Mbagala Dar es Salaam leo.
|
Umati wa
Wananchi ukiwa katika uzinduzi wa kampeni wa Chama cha ACT-Wazalendo
uliofanyika viwanja vya Zakhem Magala Dar es Salaam leo August 30,2015.
Chama cha
ACT wazalendo ni chama cha pili cha siasa na cha kwanza kwa vyama vya upinzania
kwa kusimamisha wagombea ubunge katika majimbo mengi zaidi ambapo kimeweza
kusimamisha wagombea katika majimbo 219 kati ya majimbo 265 ya jamhuri ya
muungano wa Tanzania na kikiongozwa na chama cha CCM kilichosimamisha wagombea
katika majimbo yote 265 na chama cha demokrasia na maendeleo kimeshika nafsi ya
tatu kwa kusimamisha wagombea katika majimbo.
(Picha zote kwa hisani ya :-mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062}
PAPO KWA PAPO Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo
na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment