KAMPENI ZA UCHAGUZI 2015:-UKAWA na ACT- Wazalendo Kuzindua Kampeni wiki hii. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, August 26, 2015

KAMPENI ZA UCHAGUZI 2015:-UKAWA na ACT- Wazalendo Kuzindua Kampeni wiki hii.

Zitto Kabwe akihutubia wananchi katika moja kati ya mikutano ya ACT - Wazalendo .

Chama cha ACT- Wazalendo kimepanga kuzindua kampeni zake za uchaguzi Mkuu, Jumapili, Agosti 30,2015 maeneo ya Mbagala, Temeke, jijini Dar es Salaam.

 Taarifa za uzinduzi wa kampeni zilitolewa na afisa habari wa chama hicho, Abdalah Khamisi ambaye alieleza kuwa chama hicho kitaanza rasmi kuwanadi mgombea urais, Anna Mghwira na mgombea mwenza Hamad Musa.

Kiongozi Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe ambaye alikuwa mwanachama wa CHADEMA, anatarajiwa kuongoza kampeni hizo na kuwa kivutio zaidi kutokana na historia yake nzuri ya kuvumbua ufisadi pamoja na msimamo wake wa kuwatetea wananchi bungeni.

Mgombea urais wa ACT- Wazalendo, Bi. Anna Mghwira ( Pichani ) atakabidhiwa sera za chama hicho baada ya kuteuliwa na chama chake baada ya mmoja kati ya waasisi wa chama hicho, Profesa Kitila Mkumbo kukataa kugombea nafasi hiyo licha ya kuchukuliwa fomu katika ofisi za Tume ya Taifa.


Mgombea wa UKAWA pichani, Bw.Edward Lowassa akiwa katika ziara zake kbla ya kuzindua kampeni Jumamosi August 29,2015.

Chama hicho kitakuwa chama cha tatu kuzindua rasmi kampeni zake baada ya CCM iliyozindua Jumapili ya August 23, 2015 iliyopita na CHADEMA chini ya mwamvuli wa UKAWA wanaopanga kufanya uzinduzi Jumamoji hii ya August 29, 2015 kwenye viwanja vya Jangwani Jijini Dar es Salaam.


PAPO KWA PAPO Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp  +255789925630. 


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad