Baadhi ya
wananchi wakimsikiliza mgombea mwenza wa tiketi ya CCM akihutubia Jimbo la
Arumeru.
|
Baadhi ya
wananchi na viongozi wa wafugaji wa kimasai wakifuatili kutano
|
Baadhi ya
wananchi wakimsikiliza mgombea mwenza wa tiketi ya CCM akihutubia Jimbo la
Arumeru.
|
Baadhi ya
wanachama wa CCM wakimkabidhi zawadi katika mkutano wa hadhara wa mgombea
mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu.
|
Anjela
Kairuki mmoja wa wajumbe wa kamati ya kampeni ya taifa akizungumza katika
mkutano wa mgombea mwenza.
|
Burudani kwa
wananchi na mgeni rasmi katika mkutano wa hadhara moshi Mjini.
Agrey Mwanri
(kushoto) akifuraiya jambo na Bi. Ummy Mwalimu (kulia) kwenye mkutano wa B,
Samia Suluhu,
Baadhi ya
wananchi wakimsikiliza mgombea mwenza wa tiketi ya CCM akihutubia jimbo la Hai.
Baadhi ya
wanachama na wapenzi wa CCM wakiwa katika mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza
wa CCM, Bi. Samia Suluhu Arusha Mjini.
Burudani kwa
wananchi na mgeni rasmi katika mkutano wa hadhara moshi Mjini.
Na
Joachim Mushi, Arusha.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kikifanikiwa kushinda
Uchaguzi Mkuu wa Oktoba kitahakikisha mgambo wa halmashauri ya jiji
hawawasumbui kwa kamatakamata za wafanyabiashara ndogondogo ambao wengi wao ni
akinamama pamoja na vijana.
Kauli hiyo imetolewa leo na mgombea mwenza nafasi
ya urais tiketi ya CCM, Bi. Samia Suluhu alipokuwa akihutubia mkutano wa
hadhara katika mkutano uliofanyika uwanja wa Kilombero Jimbo la Arusha Mjini na
kuhudhuriwa na umati wa wanaCCM na wananchi wengine.
Akinadi ilani ya CCM alisema chama hicho
kimeandaa utaratibu mzuri wa fursa kwa akinamama na vijana wanaofanya biashara
ndogondogo hivyo itakuwa ni marufuku kwa mgambo wa jiji kukamata biashara za
akinamama na vijana wanaojitafutia ridhiki mjini. "...Iwapo CCM
itafanikiwa kuingia mjini naomba wale mgambo ambao uishi kwa kutegemea kukamata
kamata bidhaa za akinamama watafute kazi nyingine ya kufanyanya...hatutaki
mgambo wa kufanya kazi hizo ni marufuku,
"
alisema mgombea huyo mwenza wa CCM, Samia Suluhu. Alisema Ilani ya CCM imepanga
kujenga viwanda vya kuchakata madini ili kuhakikisha vijana wanapata ajira na
kuweza kukuza vipato vyao, na kufufua viwanda vilivyosimama kikiwemo cha
'General Tyre' ikiwa ni mpango wa kumaliza tatizo la ajira kwa vijana. Aidha
alisema mpango mwingine ambao upo kwenye ilani ya CCM ni kushughulikia tatizo
la mikataba ya ajira ya madereva wa magari madogo na makubwa, "..
.Tukifanikiwa
kuingia Ikulu kazi ya kwanza tutakayoipa Wizara ya ajira ni kuhakikisha
inafanya kazi ya kushughulikia mikataba ya ajira kwa madereva wa magari madogo
na makubwa," alisema Bi. Suluhu.
Aliongeza Serikali ya CCM itaunda ufuko
wa maji kuakikisha huduma za maji zinakuwa za uhakika kwani Mkoa wa Arusha
unashughuli nyingi na idadi ya watu inakuwa kila uchao.
Serikali ya CCM
imepanga kushughulikia suala la rushwa na vitendo vya ufisadi, uzembe ili
kuhakikisha kasi ya maendeleo inaongezeka.
Awali kabla ya mkutano wa Arusha Bi.
Suluhu alifanya mikutano katika majimbo ya Hai, Siha na Arumeru yaliyopo mikoa
ya Kilimanjaro kabla ya kuingia Mkoani Arusha.
Akiwa katika majimbo hayo
mgombea aliinadi ilani ya CCM pamoja na kuwanadi wagombea ubunge na madiwani wa
CCM wa maeneo hayo. Ambapo alisema Serikali ya CCM imepanga kuboresha huduma za
afya, elimu, uwezeshaji wa vijana na akinamama ikiwa ni pamoja na kutenga
shilingi milioni 50 kwa kila kijiji kwa ajili ya kuwainua akinamama na vijana.
No comments:
Post a Comment