Bwana Amos John Kaimu meneja mkuu wa
Mgodi wa Buzwagi akifunga goli kuashiria kufungua michezo hiyo.
|
Mgeni Rasmi
Kaimu Meneja wa Mgodi wa Buzwagi akikagua timu ya Star boys wakati wa mechi ya
ufunguzi.
|
Kaimu Meneja
Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Bwana Amos John
akizungumza wakati wa uzinduzi wa
mashindano hayo.
|
Kikosi cha
Timu ya Majimaji kutoka kata ya Mwendakulima.
|
Kikosi cha
Timu ya Star Boys.
|
Moja kati ya
hekaheka wakati wa mechi ya ufunguzi ambapo timu ya majimaji yenye jezi ya
njano iliibuka kidedea dhidi ya Star boys baada ya kuitandika bila huruma goli
tatu kwa moja (3-1)
|
Na Dixon
Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini aliyekuwa mkoani Shinyanga.
Mgodi wa
dhahabu wa Buzwagi kupitia idara yake ya mahusiano ya Jamii imezindua
mashindano ya mpira wa miguu na ule wa pete, kwa timu kutoka kata ya
Mwendakulima wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Ligi hiyo
ambayo imepewa jina la Mahusiano Cup 2015, ikiwa na ujumbe wa Kuhamasisha masuala ya
Usalama, Mahusiano na Maendeleo baina ya wenyeji na mgodi wa Buzwagi itahusisha
timu tisa za mpira wa miguu na timu nane za mpira wa pete, ambapo kupitia ligi
hiyo itaundwa timu moja ya kata ambayo itakuwa ikishiriki ligi za wilaya.
Akizindua
ligi hiyo Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Bwana Amos John amesema,
kupitia mashindano hayo ambayo yamelenga kujenga mahusiano baina ya Mgodi na
wenyeji kwa kuimarisha usalama na kuhamasisha shughuli za maendeleo miongoni
mwa jamii.
Aidha kaimu
meneja huyo amewaasa vijana hao kuonyesha uwezo mkubwa wakati wote wa
mashindano kwani kupitia michezo hiyo baadhi ya vijana watakaofanya vizuri
watachaguliwa kuunda timu ya kata hiyo ambayo itakuwa ikishiriki michezo
mbalimbali kwa ngazi ya wilaya.
Awali
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama, Julius Masubo Kambarage ameupongeza uongozi wa Mgodi wa Buzwagi kwa
jitihada ambazo imekuwa ikifanya katika kuhamasisha na kuchangia shughuli
mbalimbali za maendeleo ikiwemo michezo.
“Sisi kwetu
kupata mashindano kama haya ni fursa ya pekee sana katika kuhakikisha shughuli
za michezo katika halmashauri yetu zinatekelezwa. Tutakacho kifanya kwa sasa ni
kuhamasisha hizi timu zisajiliwe ili baadae ziweze kushiriki mashindano makubwa
kwa sababu miongoni mwa hawa vijana wapo wenye vipaji vikubwa ila ni fursa tu
hawajapata” Alisema Kambarage.
Kwa Upande
wake Mratibu wa Mashindano hayo ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya
Jamii Mgodi wa Buzwagi Bwana Bahati Mwambene amezitaja timu zinazoshiriki
mashindano hayo kuwa ni Tembo,Star Boys,Shehena, zote kutoka mtaa wa Chapulwa.
Timu nyingine amezitaja kuwa ni Majimaji, Unity, Budushi, za mtaa wa
Mwendakulima, na nyingine ni Israel, Busalala na Miembeni zote hizi ni kutoka
mitaa ya Busalala na Mwime.
Aidha Bwana
Mwambene amesema kabla ya Kuanza kwa mashindano hayo timu zote zimekabidhiwa
vifaa mbalimbali vya michezo kama vile seti za jezi kwa timu zote pamoja na
mipira, ambavyo amesema pamoja na zawadi za washindi vimegharimu zaidi ya
shilingi za kitanzania milioni ishirini na mbili na laki sita.
Ligi hiyo
ambayo inafanyika katika viwanja vya shule ya msingi Mwendakulima imeanza
tarehe 23 mwezi wa nane,2015 na inatarajiwa kumalizika tarehe 05 mwezi wa tisa
2015 ambapo mshindi wa kwanza kwa kila mchezo atajinyakulia kikombe pamoja na pesa
taslimu laki tatu, huku mshindi wa pili akiondoka na laki mbili na nusu na
mshindi wa tatu akiondoka na shilingi laki mbili.
PAPO KWA PAPO Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo
na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment