![]() |
|
Bi. Samia
Othuman Suluhu akipokewa na baadhi ya viongozi na makada wakiwa kwenye mkutano
huo. |
![]() |
|
BAADHI ya
wananchi na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamelazimika kuuzuia msafara
wa mgombea mwenza wa nafasi ya urais leo alipokuwa njiani akitokea Wilaya ya
Same kuelekea Wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro huku wakimuomba awasalimu na
kuzungumza nao, kabla ya kuendelea na safari yake.
Bi. Samia
Suluhu alilazimika kuusimamisha msafara wake baada ya wananchi hao kusogea
zaidi barabarani wakati akipita huku wakinyoosha mikono ya kumuomba asimame ili
azungumze nao eneo la kilometa chache kabla ya kuingia njia panda. Wananchi hao
wengi wakiwa wakinamama walimsimamisha kwa kuingia pembezoni mwa barabara
alipokuwa akipita na hivyo kulazimika kusimama kwa dakika chache na kuzungumza
nao.
Akizungumza
aliwaambia amefarijika na kuwaona na mapenzi makubwa na chama chao hivyo
kuwaeleza kuwa yeye ni mwanamke pia na anajua kwa karibu kero ambazo
wanakabiliana nazo akinamama sehemu mbalimbali na kuahidi endapo watapata
ridhaa pamoja na Dk. John Magufuli atahakikisha anasimamia vizuri utaratibu wa
kuwawezesha akinamama kupitia vikundi vya kijamii ili waweze kujikwamua
kiuchumi pamoja na familia zao.
Alisema yeye
ni mwanamke mzazi anatambua shida wanazokumbana nazo akinamama hasa kwenye wodi
za wazazi hivyo akifanikiwa kuingia madarakani atahakikisha anasimamia ipasavyo
ilani ya chama ambayo imeeleza vizuri juu ya uboreshaji huduma za afya ikiwemo
wodi za akinamama na hali ya upatikanaji madawa......BOFYA HAPA KWA TAARIFA ZAIDI.
|
![]() |








No comments:
Post a Comment