KAMPENI CCM 2015:-Dk Magufuli: Mawaziri wazembe hawana Nafasi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, August 25, 2015

KAMPENI CCM 2015:-Dk Magufuli: Mawaziri wazembe hawana Nafasi.

Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi Mishamo mkoani Katavi .

 Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli amesema akiingia madarakani mawaziri wazembe hawatakuwa na nafasi.

Akizungumza mkoani Katavi jana August 24,2015, Magufuli alisema iwapo atachaguliwa kuwa rais baada ya

uchaguzi mkuu mwaka huu atateua Baraza la Mawaziri la wachapa kazi na atakayeshindwa kwenda na kasi yake atamfukuza.


Pia, alisema ataunda baraza dogo la mawaziri ili fedha nyingine itumike kutatua kero za Watanzania na kwamba wala rushwa na mafisadi watachukuliwa hatua ikiwa pamoja na kufungwa ili wananchi waishi kwa raha.

Dk. Magufuli alitoa kauli hiyo jana wakati wa mikutano yake ya kampeni yenye lengo la kuomba kura kwa wananchi katika uchaguzi unatarajia kufanyika Oktoba 25, mwaka huu 2015 na kwamba mawaziri wake lazima wawe wachapakazi ili kutatua shida za Watanzania.

Alisema anatambua shida za Watanzania kwani amepita katika maeneo mbalimbali na kutambua mahitaji ya wananchi na hivyo baraza lake la mawaziri lazima liwajibike kutatua shida
hizo....BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.
Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi wa Mpanda wakati akiwasili kwenye viwanja vya Azimio tayari kwa mkutano wa hadhara wa kampeni za CCM ambapo alihutubia wananchi hao waliojazana kwa wingi.
Wananchi wa Mishamo wakimsikiliza Dk.John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni za CCM mkoani Katavi.
PAPO KWA PAPO Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.  

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad