Watu wanne
wamefariki papo hapo na wengine zaidi ya 40
kujeruhiwa baada ya Treini ya
mizigo,kuligonga basi kampuni ya Don’t
Worry lililokuwa likitokea mjini Tabora kuelekea Ufuruma wilayani Uyui
mkoani Tabora leo July 27, 2015 na lilipofika eneo la kivuko cha reli
eneo la Malolo manispaa ya Tabora katika kile kilichodaiwa kuwa ni uzembe wa
dereva.
Aidha kaimu
kamanda wa polisi mkoani Tabora ,Kamishina msaidizi Juma Bwire amesema kuwa
katika ajali hiyo ya basi lenye namba za usajili T568 ABP,wanaume watatu na
mwanamke mmoja wamepoteza maisha huku dereva aliyejulikana kwa jina la Kaonjo
Iddy (34) akitoroka baada ya kusababisha ajali hiyo ambapo majeruhu wamepelekwa
katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora.
Viongozi wa
shirika la reli waliofika katika eneo la ajali hiyo wamesema kuwa
madereva hawazingatii usalama wa barabarani kwani shirika la reli limejitahidi
kuhakikisha linaweka alama husika lakini kutokana na mazoea mabaya hawajali na
matokeo ni kusababisha ajali mbaya kama hiyo.
Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment