Katika nafasi hiyo, bila shaka Magufuli
atapata shida ya kuwaongoza watu wanaokifahamu vizuri chama hicho kuliko yeye
ambaye anaonekana kama ‘wakuja’.
Historia haimuoneshi kuwahi kushika nafasi
yoyote ya uongozi katika chama, ukiondoa ujumbe wake wa Halmashauri Kuu (NEC).
Lakini pia Magufuli akiwa Ikulu, itampasa
kujifunza uvumilivu, somo moja gumu sana ambalo kwa asili huwa ni kipaji.
Ingawa tunafurahi kwa sababu tunaelekea kumpata kiongozi mtendaji, lakini tuna
hofu kuu na jinsi anavyotekeleza majukumu yake, hasa ule mtindo wake wa
kuwajibisha watu jukwaani.
Rais wa nchi hapaswi kuwa mtu wa kukurupuka,
kwa sababu ya unyeti wa nafasi yake pamoja na madaraka yake makubwa. Kama
hatakuwa mtu wa kusikiliza, kutafakari na kushauriwa, ipo hatari ya nchi
kushuhudia maamuzi yatakayoandika historia.
Lakini pia Magufuli atapaswa kujifunza
diplomasia. Siasa za nje ni vitu vya msingi sana katika ujenzi wa taifa lolote.
Historia haimuoneshi kama mtu mwenye kufahamiana na wanasiasa wa nje, kitu
ambacho kwa kiongozi wa ngazi yake ni muhimu sana.
Vyovyote iwavyo, urais wa Magufuli una vitu
vingi vya msingi alivyopaswa kuwa anavijua, ambavyo bahati mbaya atakwenda
kujifunzia akiwa Ikulu na hili siyo jambo dogo kama tunavyofikiria.
Source:-Global Publishers.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment