![]() |
Kikosi cha
Yanga SC kilichoanza kwenye mchezo wa Jana July 26,2015 dhidi ya Khartoum National Club Kwenye Kagame CUP 2015.
Hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na
Kati (Kagame Cup 2015) inatarajiwa kuanza kesho Jumanne July 28,2015 kwa michezo miwili
kuchezwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mchezo wa kwanza utakua ni kati ya Mabingwa mara tatu wa michuano hiyo
timu ya APR ya Rwanda itakayotoshuka dimbani saa 7:45 mchana kucheza na vijana
wa Kwesi Appiah timu ya Al Khartoum kutoka nchini Sudan.
Saa 10:15 kamili jioni, Gor Mahia mabingwa wara tano wa michuano ya
Kagame watashuka dimbani kucheza na Malakia kutoka Sudan Kusini, viingilio vya
michezo hiyo ya jumanne cha chini kitakua ni elfu tatu (3,000) na kiingilio cha
juu kitakua ni elfu kumi na tano (15,000).
Robo fainali zitaendela siku ya jumatano July 29,2015, ambapo michezo miwili itachezwa
katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam huku macho na masikio ya wapenzi wa
mpira Afrika Mashariki yakielekezwa kwa mchezo kati ya Azam FC dhidi ya Yanga
SC.
Kabla ya mechi hiyo ya wapinzani wa soka nchini Tanzania kuchezwa majira
ya saa 10 jioni, mchezo wa kwanza utazikutanisha timu za KCCA ya Uganda dhidi
ya Al Shandy kutoka nchini Sudan.
Viingilio vya mchezo wa siku ya jumatano, kiingilio cha chini ni shilingi
elfu tano (5,000) na kiingilo cha juu kitanua ni elfu ishirini (20,000).
Katika hatua hiyo ya robo fainali endapo timu zitacheza kwa dakika 90 na
mchezo kumalizika kwa sare, hatua itakayofuata ni kumpata mshindi kwa matuta
(penati).
Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Monday, July 27, 2015
Home
MICHEZO
ROBO FAINALI KAGAME CUP 2015:-Ni kesho July 28, 2015 kati ya huku Yanga na Azam FC Jumatano July 29, 2015.
ROBO FAINALI KAGAME CUP 2015:-Ni kesho July 28, 2015 kati ya huku Yanga na Azam FC Jumatano July 29, 2015.
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment