Meneja
Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi akikabidhi zawadi
ya T-shirts kwa mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Imani Makongoro.
|
Baadhi ya
waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Na Andrew Chale, modewjiblog
Msimu mpya wa Soka 2015/16,
unatarajia kuanza rasmi Jumapili ijayo kwa kushuhudia ligi mbalimbali Duniani
zikichezwa na kurushwa moja kwa moja kupitia SuperSport
ambayo imejipanga kukuletea burudani kabambe kwa mashabiki wa soka barani
Afrika.
Meneja uendeshaji wa Multichoice
Tanzania , Ronald Baraka Shelukindo mapema jana akizungumza na vyombo vya
habari amebainisha kuwa, Wateja wa DStv wakae tayari msimu huu kwenye Ulimwengu
wa Mabingwa ambapo timu mbalimbali zimejiimalisha katika kuakikisha
zinatwaa ubingwa.
“Ligi ya mwaka zitakuwa za kasi na kuvutia
kwa kila timu. Barcelona wanajiandaa kutawala dunia kwa mara nyingine, huku
Manchester United wanahitaji kurudisha kiti chao cha Ubingwa Uingereza.
Jose Mourinho analenga kuhakikisha Chelsea inabaki juu,
wakati huo huo , Hispania inajiandaa kuhakikisha wanashinda kwa mara ya tatu
kombe la Euro 2016.” Ameeleza Baraka Shelukindo.
Ameogeza kuwa, Watazamaji wa
SuperSport watakuwa na nafasi ya kipekee kushuhudia mechi
kwenye ubora wa HD, ikiwa ni pamoja na michuano ya Ligi Kuu ya
Uingereza (EPL) , Ligi ya Hispania (La Liga) , Ligi ya Mabingwa wa Ulaya(UEFA)
na Ligi ndogo ya Ulaya ( Europa) ,mechi za FIFA za kirafiki za kimataifa
na Klabu Bingwa ya Dunia , Kombe la Ujerumani , Kombe la Mfalme
Hispania (Copa Del Rey) , Kombe la FA na zaidi.
Kwa upande wake, Meneja Uhusiano wa
Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi anaeleza kuwa, Katika msimu huu ,
Ulimwengu wa Mabingwa itakuwa ikionyesha mechi zaidi ya 900 za kimataifa.
Wateja wa DStv Compact Plus wataweza kufurahia baadhi ya mechi zaidi ya 450
‘live’, huku Wateja wa DStv Premium watazawadiwa mechi zote ‘Live’
zitakazorushwa katika chaneli zote za SuperSport .
“Kuanzia msimu huu na kuendelea,
vituko vyote vya Ligi Kuu ya Uingereza vitakuwa vikiletwa kwenu
kupitia SuperSport 5 ( SS5 ) inayopatikana kwenye kifurushi cha Premium.
SS5 sasa itakuwa ni nyumba ya soka la Afrika kwa ligi kuu ya Uingereza
huku ikijumuisha mechi 3 ‘Live’ kila Jumamosi na Jumapili.
Kuambatana na mechi kutakuwa na vipindi maalum vya soka kama
PLTV Kick Off, Match Day Live, Fan Zone, Saturday/Sunday Review, Football
Today, Classic Matches, Netbusters na Mech za Wiki” Amebainisha Barbara
Kambogi.
Moto wa La Liga utawashwa ndani
ya SuperSport 3 ( SS3 ). Chaneli hii itakuwa inakuletea mechi hadi tatu
za ligi ya Hispania ‘ Live’ kwa siku ya Jumamosi na Jumapili .
Wateja wa
DStv Premium na Compact Plus watapata nafasi ya kuangalia mechi za
michuano ya Kombe la mashindano Uingereza ndani ya SS3 sambamba na mechi
za Jumamosi mchana za Ligi kuu ya Uingereza , mbadala wa mechi
inayorushwa ndani ya SS5, pamoja na Ratiba zote za Jumatatu usiku
na vipindi vya mahojiano vya studio.
Pamoja na Mechi za ‘Live’ ndani ya SS3
, itakuwa inakuonyesha vipindi muhimu vya shoo za magazeti ,
yanayojiri ndani ya La Liga, pamoja na vipindi maalum vya ligi za
soka .
Makombe yote ya mpira wa miguu, Mabingwa wa Ulaya na Ligi ya
Europa, Kombe la FA , Kombe la Mfalme Hispania (Copa Del
Rey), Kombe la Ujerumani , Euro 2016 na mechi za kirafiki za kimataifa
zitaendelea kutapatikana kwenye SS3 .
Kwa habari zaidi za michezo na ratiba za
mechi kwenye SS5 na SS3, tafadhali tembelea www.supersport.com
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment