Baadhi ya
waandishi wa habari wakimsikiliza Kaimu kamishna wa uhamiaji Abasi Irovya jijin
Dar es Salaam….Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
IDARA ya
Uhamiaji nchini imetoa onyo kwa raia wa kigeni watakaobainika kuwa na
vitambulisho vya kupigakura baada ya kubaini raia hao zaidi ya 2,000 kuwa na
vitambulisho hivyo katika msako unaofanywa na maofisa wao kwenye miji iliyo
mipakani hapa nchini.
Idara hiyo
imesema tayari imeshaanza kuwachukulia hatua za kisheria raia hao ikiwa ni
pamoja na kuwanyang’anya vitambulisho hivyo, kuwaondoa nchini baadhi na wengine
kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.
Mikoa ambayo
raia hao wamebainika kujiandikisha kwenye daftari hilo na idadi yake kwenye
mabano ni pamoja na Kagera (708), Mara (619), Tanga (348), Kigoma (254), Rukwa
(13) na Kilimanjaro (12).
Mikoa
mingine ni Ruvuma (9), Geita (6), Shinyanga (7), Mtwara (3), Pwani (2), Dar es
Salaam (65), Mbeya na Morogoro mmoja kila mkoa.
Msemaji Mkuu
wa Idara ya Uhamiaji nchini, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Abbas Irovya alisema
jana jijini Dar es Salaam kuwa, maofisa wa Idara hiyo wanaendelea na uchunguzi
na watakapowabaini wengine hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Aidha
alisema ni kosa kisheria kwa raia yeyote wa kigeni kujiandikisha ili apate
kitambulisho cha kupiga kura na hivyo kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa
kuwafichua raia hao.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Friday, July 31, 2015
BVR TANZANIA:-Kagera kinara kwa Wageni 708 matatani kwa kujiandikisha BVR.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment