Michuano imefikia hatua ya nusu fainali baada
ya kufanyika robo fainali zenye mvuto.
Nusu Fainali hizi zitakuwa kama marudio ya
Mechi za Makundi kwani Timu hizo zilipambana kwenye Makundi yao kwa Azam FC
kuifunga KCCA 1-0 kwenye Kundi C na toka Kundi A Gor Mahia kutoka 1-1 na Al
Khartoum.
NUSU
FAINALI KAGAME CUP 2015.
Ijumaa
Julai 31, 2015 .
Al Khartoum v Gor Mahia [Mechi Na 27]
KCCA Vs Azam FC [Mechi Na 28]
Jumapili
Agosti 2,2015.
MSHINDI
WA TATU
Al Khartoum/Gor Mahia v KCCA/Azam FC
FAINALI
KAGAME CUP 2015.
Al Khartoum/Gor Mahia v KCCA/Azam FC
Zaidi ya heshima ya kikombe kinachoshindaniwa
kwenye haya mashindano pia kuna donge nono ambalo limewekwa kwa ajili ya Klabu
itakayobeba ndoo.
Kama ulikua hujui taarifa ikufikie kwamba
bingwa wa Kagame Cup 2015 ataondoka na pesa kiasi cha $10,000 pamoja na kikombe.
Tuendelee kufatilia mashidano haya hadi tujue nani ataondoka na kitita hiki.
Heshima ya timu pamoja na pesa hizi zinaweza
kwa kiasi kikubwa kusaidi uendeshaji wa klabu na mambo mengine.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment