|
Meneja wa
Usimamizi wa Biashara za kadi (ATM) na Huduma za Ziada, Chihoma Chihoma
akizungumza na wanahabari (hawapo pichani)...na hapo akionesha mfano wa
MasterCard mpya itakavyokuwa. |
|
Chihoma
(katikati) akizungumza na wanahabari.
BENKI ya
National Microfinance (NMB) inatarajia kuzindua huduma mpya za mashine ya ATM
za MasterCard zijulikanazo kama World Rewards,Titanium na Tanzanite.
Akizungumza
leo katika kikao kifupi na wanahabari kwenye Ofisi za GEPF Victoria jijini Dar,
meneja wa usimamizi wa biashara za kadi za ATM na huduma za ziada, Chihoma
Chihoma, amesema wanatarajia kuzindua huduma hizo za kibenki kutokana na
mahitaji ya wateja kuwa juu na kuona vyema kuongeza wigo ili kuwawezesha
upatikanaji wa huduma bora na za haraka.
Alisema kuwa
huduma hiyo mpya itakapozinduliwa itawawezesha wateja wa NMB kutoa kiasi
kikubwa cha fedha kutoka katika ATM za MasterCard tofauti na hivi sasa. Kwenye
kadi hizo mpya, mteja ataweza kutumia katika manunuzi ya bidhaa na pia kulipia
huduma mbalimbali na mteja anaweza kutoa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni
moja kila katika ATM tofauti.
Aliongeza
kuwa NMB Mastercard ni rahisi kutumika na ni salama kutokana na tekinolojia
yake iliyotumika kutengenezea hivyo wateja wakae tayari kupokea huduma hiyo
mpya hivi karibuni.
(PICHA/HABARI:
DENIS MTIMA/GPL)
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|





No comments:
Post a Comment