PICHA ZIARA YA KINANA NGARA/KAGERA:- Awahutubia wananchi wa Ngara mjini pamoja na kuitaka Serikali kurahisisha utoaji wa leseni kwa wafanyabiashara , madereva wa magari na bodaboda. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, June 14, 2015

PICHA ZIARA YA KINANA NGARA/KAGERA:- Awahutubia wananchi wa Ngara mjini pamoja na kuitaka Serikali kurahisisha utoaji wa leseni kwa wafanyabiashara , madereva wa magari na bodaboda.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Abdulrhaman Kinana akiwahutubia wananchi wa Ngara mjini jana June 13,2015 kwenye uwanja wa posta ya zamani,Kinana ameitaka Serikali kurahisisha utoaji wa leseni kwa wafanyabiashara , madereva wa magari na bodaboda badala ya kuacha watu wanasumbuka kutafuta leseni umbali mrefu tena kwa gharama kubwa.

 Kinana amesema kuwa  moja ya ombi la wananchi hao ilikuwa ni kuomba kurahisishiwa kupata leseni ili kuondoa usumbufu wanaoupata sasa.Alisema Serikali lazima iweke mazingira mazuri ya kutoa leseni kwa wananchi wakiwamo wafanyabishara na madereva bodaboda huku akieleza hakuna sababu ya kutumia gharama kubwa kwa ajili ya leseni.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa mji wa Ngara Mjini kwenye mkutano wa hadhara,Nape Nnauye alisema kuwa hakuna
sababu ya Watanzania kuingia kwenye mpasuko kwa sababu ya mchakato wa
katiba mpya na kuashauri ni vema mjadala ukafungwa kwenye nyumba za
ibada. Amesema inasikitisha unapoona baadhi ya viongozi wa dini badala
ya kuhubiri neno la Mungu na kuwaunganisha Watanzania wanatumia nafasi
yao kuwagawa wananchi kwa sabababu ya Katiba mpya.....


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na mhandisi wa kampuni ya kichina ya TKPE Bw.Ton Minyang wakati alipokagua ujenzi wa  Mtambo wa umeme  vijijini REA jana June 13,2015 ,unaojengwa katika kijiji cha Djuruligwa kata ya Kabanga wilayani Ngara.


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pamoja na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kagera Mama Constansia Buhie wakizikusanya kadi  mbalimbali za wafuasi wa upinzani na kuzikabidhi kwa viongozi hao wa CCM,ikiwa ni ishara ya kujiunga na chama hicho cha CCM.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua rasmi Chanjo ya  watoto kuzuia maambukizi ya magonjwa katika kata ya Nyakisasa kijiji cha Kashinga akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani Ngara mkoani Kagera jana June 13,2015,lengo la ziara hiyo likiwani ni kukagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2010 na kuhimiza uhai wa chama, Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na ktibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na viongozi mbalimbali wa CCM  kutoka mkoa wa Kagera.….PICHA NA MICHUZI JR-NGARA...KUONA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad