![]() |
|
Mbunge Bunda
na Waziri wa Chakula na Kilimo,Bw. Stephen Wassira akionyesha fomu baada ya kupata wadhamini
122 mjini Bukoba.....Mwingine ni Mbunge wa Bukoba Vijijini Jasson Rweikiza. |
![]() |
| Stephen Wassira akisaini kitabu katika Ofisi za CCM ya Bukoba, Kulia kwake ni Mwenyekiti wa chama wa Wilaya hiyo Novatus Nkwama. |
![]() |
|
Wadhamini
katika picha pamoja na Stephen Wassira na viongozi wengine.KUONA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
KUTOKA
GAZETI LA NIPASHE
Waziri
Stephen Wassira ambaye pia ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania amesema yeye ndiye anayefaa kuwa rais wa nchi kwa sababu
anaichukia rushwa na hana kashfa yoyote.
Alisema nchi
hii kwa sasa imejaa wala rushwa na kwamba yeye ataikomesha kwa sababu
anaichukia wala hajawahi kuiomba au kuipokea, huku akisema kuwa kuna wanachama
wenzake, ambao ni wala rushwa wakubwa na kila kashfa wanaguswa lakini sasa wanataka
waingie Ikulu kwa kutumia rushwa waliyoivuna wakiwa madarakani.
Aidha,
alisema akibahatika kuingia tano bora na kisha tatu bora na badaye akapeperusha
bendera ya CCM kama mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama hicho, ni lazima
viongozi wa Ukawa watajinyonga kwa sababu wanamtambua jinsi alivyo na uwezo.
“Ukienda
hospitali utakutana na rushwa, polisi rushwa na mahakamani rushwa… Rushwa
imeanza zamani maana hata yule aliyekuwa akibeba mikoba ya Yesu, lakini
alivyopewa vipande 30 vya fedha akamsaliti Yesu, kwa hiyo rushwa ni tatizo haikuanza leo, bali ya leo imezidi sana, ipo
nyingine ya mikataba mibovu, manunuzi, sasa akiwa Rais ambaye ni mla rushwa
atawaonea aibu wenzake.”—Waziri Wassira.
Alisema
atahakikisha jembe la mkono kwa wakulima linakuwa historia, ikiwa ni pamoja na
kuongeza ajira kwa vijana, kingine ni kuboresha elimu ya sayansi kwa wanafunzi
wa sekondari.
|










No comments:
Post a Comment