|
Nigeria
imeanzia kileleni mwa Kundi G baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Chad mechi
ya ufunguzi kuwania kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika 2017 jana uwanja wa
Ahmadu Bello,Kaduna.
Shukrani
kwao, wafungaji wa mabao hayo, Gbolahan Salami dakika ya 63 na O Ighalo kwa
penalti dakika ya 80.
Mechi
nyingine ya Kundi G inazikutanisha wenyeji Misri dhidi ya Tanzania leo mjini
Alexandria.
Katika mechi
nyingine za jana June 13, 2015, Algeria iliifumua mabao 4-0 Shelisheli, Mali
imeifunga 2-0 Sudan Kusini, Senegal imeifunga 3-1 Burundi na Burkina Faso
imeichapa 2-0 Comoro.
Afrika
Kusini imelazimishwa sare ya 0-0 na Gambia, Cape Verde imeichapa 7-1 Sao Tome,
Angola imeipiga 4-0 Jamhuri ya Afrika ya Kati, Uganda, imeifunga Botswana mabao
2-0, Zambia imelazimishwa sare ya 0-0 Guinea-Bissau na Malawi imefungwa 2-1 na
Zimbabwe.
Mechi za
juzi June 12, 2015, Tunisia iliifunga mabao 8-1 Djibouti, Morocco ilishinda bao
1-0 dhidi ya Libya na Swaziland walishinda 2-1 dhidi ya Guinea.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori
inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment