UTAFITI:-Hii ndio Mikoa 7 Nchini Tanzania yenye Maendeleo duni ya Watu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 08, 2015

UTAFITI:-Hii ndio Mikoa 7 Nchini Tanzania yenye Maendeleo duni ya Watu.

Ripoti imetaja mikoa 7 yenye maendeleo duni ya watu Tanzania. DODOMA, KIGOMA, SINGIDA, KAGERA, TABORA, SHINYANGA na PWANI ndio mikoa inayoongoza kwa maisha duni ya watu Tanzania.

 Hayo yamo katika ripoti iliyozinduliwa na serikali juma lililopita,ripoti hiyo pia imeitaja mikoa inayoongoza kwa hali bora za maisha ya watu Tanzania kuwa ni: DAR ES SALAAM, ARUSHA, KILIMANJARO, IRINGA, RUVUMA, MBEYA na TANGA.

Vigezo vilivyotumika katika utafiti uliozaa ripoti hiyo ni, wastani wa muda wa kuishi (Life expectancy, max 83.6 - min 20), expected years of schooling, upatikanaji wa maji safi na salama, umeme, lishe, vifo vya mama wajawazito na watoto, maendeleo ya jinsia.

Vigezo vingine ni, mazingira, kipato, umaskini, uhuru na upatikanaji wa mahitaji ya msingi kama chakula, maji na nyumba.

Utafiti huo ulifanywa na Economic & Social Research Foundation (ESRF) kwa kushirikiana na; - National Bureau of Statistics (NBS). - The Office of the Chief Government Statistician of Zanzibar. - The Department of Economics of the University of Dar es Salaam na kudhaminiwa na UN. 

Source; The Citizen 

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad