UKWELI NA UWAZI:-Huu ndio Utajiri wa Zitto Kabwe. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, April 06, 2015

UKWELI NA UWAZI:-Huu ndio Utajiri wa Zitto Kabwe.

Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT - Tanzania, Zitto Kabwe ameweka hadharani utajiri wake akisema ana fedha taslimu Sh18 milioni na nyumba mbili zenye thamani ya Sh223 milioni zilizopo Mwandiga, Kigoma.


Zitto alitangaza mali hizo ikiwa ni sehemu ya kutimiza matakwa ya katiba na kanuni za maadili ya viongozi wa chama hicho kinachojinasibu kwa kuenzi sera ya ujamaa wa Hayati Mwalimu Julius Nyerere ya mwaka 2015.

Kwa mujibu wa fomu hiyo aliyoijaza, Mbunge huyo wa zamani wa Kigoma Kaskazini (Chadema), hadi Machi 29,2015 alikuwa pia anamiliki fedha katika akaunti mbalimbali za benki; CRDB ana Sh5.98 milioni, Dola za Marekani 188 (Sh347,000) na Euro 495 (Sh965,250).

Katika akaunti ya Benki ya NMB anamiliki Sh800,000 wakati katika Benki ya Stanbic anamiliki akaunti ya familia yenye Dola za Marekani 1,000 (1.85 milioni) akiwa na asilimia 40 na dada yake Thabitha Salumu.

 Mbali na fedha, Zitto anamiliki gari aina Rand Rover Freelander yenye thamani ya Dola za Marekani 40,000 (Sh74 milioni).

Akizungumzia nyumba alizonazo, Zitto alisema moja ina thamani ya Sh180 milioni na nyingine Sh43 milioni zote zikiwa mkoani Kigoma. 

Source:-mwananchi.co.tz.

Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila tukio/stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad