PICHA / HABARI:-Hii ajali abiria waliokuwemo kwenye taxi wala Dereva hata hawakujua hiki kingetokea, #RIP kwa watu wetu waliofariki. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, April 27, 2015

PICHA / HABARI:-Hii ajali abiria waliokuwemo kwenye taxi wala Dereva hata hawakujua hiki kingetokea, #RIP kwa watu wetu waliofariki.

Ajali hii ya kusikitisha imetokea mjini wa Kano, Nchini Nigeria ambapo Watu saba wamefariki kutokana na  kuanguka kwa daraja la waenda kwa miguu lililokuwa likiendelea kujengwa katika barabara.

 Mara nyingi ujenzi ukiwa unaendelea kwenye barabara kunakuwa na vibao vya maelekezo lakini watu wengi huwa hawazingatii maelekezo, ndicho ambacho kimetokea kwenye hii ajali ya Nigeria.

Polisi wanafanya uchunguzi wa tukio hili.. ambapo..“Mafundi waliokuwa wanajenga waliwakataza watu wasipite na magari chini ya daraja kwa sababu bado kazi ya ujenzi ilikuwa ikiendelea,lakini huyo dereva wa taxi alikiuka agizo hilo.. alikuwa anakatisha na gari ikiwa na abiria, daraja likaanguka.. wamefariki watu saba..“– Magaji Majiya, msemaji wa Jeshi la Polisi.

Picha nyingine za ajali hiyo hizi hapa..
Pata Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati  wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad