KIBARUA KIGUMU:-Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yasogeza mbele kwa wiki moja siku ya kuanza kuandikishaji wapiga kura kwa mfumo wa (Biometric Voter Registration – BVR), Sasa ni Februari 23,2015. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, February 14, 2015

KIBARUA KIGUMU:-Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) yasogeza mbele kwa wiki moja siku ya kuanza kuandikishaji wapiga kura kwa mfumo wa (Biometric Voter Registration – BVR), Sasa ni Februari 23,2015.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),Jaji Damian Lubuva akizungumza wakati wa mkutano na Viongozi wa Vyama vya Siasa uliofanyika Februari 12,2015  kwenye Ukumbi wa JB Belmonte,Jijini Dar es salaam.Wengine pichani ni Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw.Julius Malaba na kulia ni Kamishina wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Prof. Amon Challigha.

 Zikiwa zimebaki siku Kama 70 hivi kupia kura ya maoni Katiba inayopendekezwa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ambayo inajukulu la kufanikisha zoezi hilo, imesema imamatumaini kuwa litakamilika.

 Hata hivyo, pamoja na NEC kusema hivyo, bado inaonekana inakabiliwa na changamoto nyingi kulifanikisha.

Kwa mujibu wa sheria namba tatu ya mwaka 2014 ya kura ya maoni,  jambo la kwanza kufanyika ni uboreshaji wa daftari la wapigakura, elimu kwa umma kwa miezi miwili na kampeni kwa mwezi mmoja.

Tayari serikali imetangaza kuwa kura ya maoni kwa Katiba inayopendekezwa itafanyika Aprili 30, mwaka huu 2015.

Moja ya mitihani hiyo ni kukamilisha zoezi la uandikishaji wa wapiga kura uliotakiwa kuanza Februari 16, mwaka huu, kwa kuanza na mikoa mitatu ya Njombe, Ruvuma na Lindi, ambalo lingefanyika  kwa siku saba kwa kila mkoa na kwamba ni matumaini ya Tume kuwa zoezi litakamilika kwa mikoa yote kabla ya Aprili 29, mwaka huu.
Sehemu ya Viongozi wa Vyama vya Siasa waliohudhulia Mkutano huo wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),Jaji Damian Lubuva (hayupo pichani) leo kwenye Ukumbi wa JB Belmonte,Jijini Dar es salaam.

Leo hii Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania (NEC), imesogeza mbele zoezi hilo la uandikishaji wa wapiga kura katika Daftari la Kudumu la Wapiga kura hadi Februari 23, mwaka huu 2015, huku vyama vya siasa vikilalamikia kutoshirikishwa na utendaji kazi wa kusuasua wa Tume hiyo.

Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva, alitangaza hatua hiyo Februari 12,2015 wakati wa mkutano wa pamoja baina ya vyama vya siasa na Nec kujadili zoezi hilo la uandikishaji wa wapigakura katika Daftari la Kudumu la Wapiga kura chini ya mfumo wa Biometric Voter Registration (BVR).

Anasema awali NEC ilipanga zoezi hilo lianze Februari 16, mwaka huu, lakini kutokana na maoni ya wadau kutaka lisogezwe mbele, wameamua litaanza Februari 23, mwaka huu, ili kutoa nafasi kwa vyama vya siasa kuweka mawakala katika vituo mbalimbali vya uandikishaji.

Hata hivyo, alipoulizwa zoezi hilo litaendelea hadi wakati gani, anasema kwa sasa ni vigumu kueleza kwa kuwa vifaa (BVR kits) vilivyopo ni 250, na matarajio ni kupata vifaa 7,750 ambavyo vitawezesha zoezi hilo kukamilika nchi nzima kwa muda mfupi.

Tumeongeza muda wa wiki moja ili kutoa nafasi kwa vyama vya siasa kuweka mawakala na kuelimisha wananchi umuhimu wa kujitokeza kuandikishwa…hatuna haja ya maandamano njooni ofisini tutawasikiliza kama tulivyowasikiliza kwenye ombi la kusogeza mbele muda,” alisema Jaji Lubuva.

Wakizungumza katika mkutano huo, viongozi wa vyama vya siasa waliitaka NEC kuwa wazi na kutoa taarifa kwa wakati na majibu mazito kwa maswali yanayoulizwa na siyo kutoa majibu mepesi kwa maswali magumu.

Pia viongozi hao waliitaka Tume hiyo kuweka wazi ni kiasi gani cha fedha wamepata na matumizi ya vyombo vya dola katika ulinzi wakati wa uandikishaji ambao utatisha au majeshi yatatumiwa kwa malengo ya kisiasa.


UNGANA  NASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
 
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad