HABARI / PICHA:- CHADEMA yasema Shule za Kata Tanzania ni Matabaka na Ni Mizigo..’’ - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, February 09, 2015

HABARI / PICHA:- CHADEMA yasema Shule za Kata Tanzania ni Matabaka na Ni Mizigo..’’

Naibu Katibu mkuu wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA,Upande wa  Zanzibar,Bw. Salum Mwalimu akivishwa skafu na kamanda wa skauti Nelson Felix alipokuwa amewasili Jana Februari 08,2015,Jimbo la Muleba Kusini  mkoani Kagera kuhutubia Wananchi wa jimbo hilo..Picha/Habari Na:-Shaaban Ndyamukama.

 Wananchi wilayani Muleba mkoani Kagera wameshauriwa kuhakikisha wanajiamini  na kusimamia rasilimali zao zikiwemo zinazotoka ndani ya ziwa victoria ili waweze kuzitumia kwa manufaa yao na kizazi kijacho.

Katibu wa Baraza la Wazee (CHADEMA) ngazi ya Taifa ,Bw.Rodrick Tutembeka amesema hayo jana Februari 08,2015, katika mkutano  wa Hadhara uliofanyika Katika Jimbo la Muleba Kusini na kudai kuwa baadhi ya rasilimali kama ardhi  zinaporwa na wenye nyadhifa Serikalini.

Bw.Rutembeka amesema kuwa kinachohitajika ni kupaza sauti zao kudai haki ya umilikaji wa ardhi kwa usawa na kuwekeza ndani ya ziwa ili kujipanua kiuchumi kwa kuvua samaki na dagaa na kuuziana wao kwa wao na kujiongezea mapato.

Amesema kuwa jambo lingine ni kuishinikiza serikali kupitia viongozi waadilifu wa kisiasa na wenye utashi wa kutetea haki na maslahi ya taifa kutumia ziwa victoria kusambaza huduma ya maji vijijini ili kuondoa usumbufu uliopo.

Aliongeza kuwa wilaya ya Muleba inazo rasilimali ambazo viongozi waadilifu wakipatikana kupitia vyama bora na imara vya kisiasa umaskini kwa watanzania unaweza kuwa ndoto kwani wanaweza kuelimishwa kujikwamua kiuchumi.

Wakati mkutano huo ukitarajiwa kuwa na ulinzi kutoka Jeshi la Polisi  Muleba,hawakuweza kuonekana badala yake walijitokeza vijana wa Chama cha Maskauti wa wilaya hiyo kuimarisha usalama wakati mkutano ukiendelea.

Makamanda wa skauti   walifika katika mkutano na kuzua taflani kwa wananchi kwa kujiuliza kulikoni mara kikosi cha maaskauti kilipoingia uwanja wa red cross na kujipanga kila kona wakati viongozi wakiwa majukaani wakihutubia.

Mara baada ya kuwasili uwanjani hapo na wananchi kuanza kujiuliza maswali kadhaa aliyekuwa akihutubia Katibu wa baraza la Wazee (Chadema ) ngazi ya Taifa Bw. Rodrik Rutembeka alitoa nafasi kwa vijana hao kueleza kilichowaleta

Kiongozi wa makambanda hao Godleva Kabalila alisema walikuja kuimarisha ulinzi ikiwa ni pamoja na kueleza umma kuwa wanajukumu la kudhibiti vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto katika utumiaji wa dawa la kulevya.

Alisema Februari 14 mwaka huu 2015, Vijana hao watakutana na wenzao kutoka Bukoba vijijini na Uganda katika kongamano lasiku mbili kujadili mafanikio na changamoto za kuunda chama hicho mwaka mmoja uliopita.

Hata hivyo  viongozi wa Chadema pamoja na wafuasiwa wao wakiongozwa na Naibu katibu Mkuu wa Chadema kutoka Zanzibar,Bw. Salumu Mwalimu waliendesha harambee na kuwchangia vijana hao Sh 200, 000 ilikufanisha kongamano lao.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Upande wa  Zanzibar,Bw. Salum Mwalimu akiendesha harambee ya kuchangisha Sh 200,000 kwa ajili ya kuwezesha Vijana wa Skauti wilayani Muleba mkoani Kagera kushiriki  kongamano la kutathimini vitendo vya ukatili dhidi ya watoto litakalojumuisha maskauti 150 kutoka Bukoba vijijini na Uganda Februari 14 mwaka huu,2015 wilayani Muleba...Picha/Habari Na:-Shaaban Ndyamukama.


Naibu katibu mkuu wa Chadema upande wa Zanzibar Bw.Salum Mwalimu amesema Wananchi hawana budi kuwapeleka shule katika wilaya na mikoa mbali mbali na kuepuka sera za shule za sekondari za kata zenye matabaka.

Amesema shule hizo zimejengwa zikiitwa shule mkombozi kwa wazazi lakini ubaguzi wa kimatabaka umeanza kuonekana baada ya wanafunzi kushindwa kuitambua jografia ya nchi yao na makabila na tamaduni tofauti za nchi yao.

Ukichukulia mkazi wa Izigo shule ya msingi na sekondari ni hapo hapo, chuo cha ualimu ni kijiji  jirani cha Katoke na kuajiriwa ni Izigo kuoa ama kuolewa Izigo na makazi yake Izigo kwanini shule hizi zisiitwe mizigo?Alihoji Mwalimu.

Pamoja na hayo kawataka wananchi kujiandikisha katia daftari la kudumu la wapiga kura na kuwasihi kutojitokeza katika kura ya maoni ya Katiba inayopendekezwa kwa kuwa imesusiwa na Vyama vinavyounda UKAWA.
UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad