Waziri wa
Nishati na Madini ,Bw.George Simbachawene amesema kuwa watanzania wamuamini
ataendeleza kwa kasi ile ile katika kuwafikishia wananchi maendeleo kupitia
sekta za nishati na madini.
Hayo ameyasema leo Januari 26,2015,wakati alipoanza kazi rasmi katika Wizara hiyo akichukua
nafasi ya Profesa Sospeter Muhogo aliyejiuzulu wiki iliyopita,amesema kila mtu
sio mkamilifu hata mitume watu wengine hawakumuamini.
Bw.Simbachawene amesema ana uzoefu wa kufanya kazi na kuachana na vyeti kwani
vyeti ni ziada lakini kalama ya uongozi ndiyo inayohitajika.
Aidha amesema wanaotilia shaka uteuzi wake watakuwa na kigezo lakini kila mtu
hawezi kuamini kila binadamu ana mapungufu kwa namna anavyoona mtu.
Simbachawene amesema atafuatilia usiri wa mikataba lakini sasa anasoma
mazingira kwanza na kuweza kuweka bayana suala hilo.
“Niko hapa watu waniamini kutokana na kazi zangu na watanzania waniamini niweze
kufanya kazi niliyoaminiwa kwa niaba ya watanzania wenzangu”amesema
Simbachawene.
|
No comments:
Post a Comment