TEKNOLOJIA:-Facebook yapotea kwa dakika 40 Duniani. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, January 27, 2015

TEKNOLOJIA:-Facebook yapotea kwa dakika 40 Duniani.

Mtandao wa kijamii wa facebook ulikuwa hauingiliki katika maeneo mengi Duniani mapema leo Januari 27,2015 kabla ya huduma zake kurudi.


Mamilioni ya watumizi wa mtandao wa facebook walishindwa kuingia katika akaunti zao.

Wateja wake katika mataifa mengine walishindwa hata kutumia hudumu ya Instagram.
Facebook ilisema kuwa wahandisi wake ndio walioababisha tatizo hilo, na kukana madai kwamba kundi moja linalotekeleza uhalifu wa mitandaoni lilihusika.

''Awali watu wengi walikuwa hawawezi kuingia katika akaunti zao za mitandao ya facebook pamoja na huduma ya Instagram'', msemaji wa facebook aliiambia BBC.

''Hili halikuwa shambulizi kutoka kwa watu wengine lakini lilitokea baada ya kufanya mabadiliko ambayo yaliathiri mpangilio wa mfumo wetu''.

Tuliharakisha na kutatua tatizo hilo na sasa huduma zote zimerejelea asilimia 100 kama kawaida

Mitandao hiyo ilitoweka kwa takriban dakika 40 kabla ya kurudi.

Programu ya mtandao unaowaunganisha wapendanao Tinder ambayo hutegemea facebook ili kutoa huduma zake pia iliathiriwa na tataizo hilo.

Kundi moja la uhalifu wa mitandano kwa jina Lizard Squad liliandika ujumbe kwa twitter kuhusu hudumu hiyo kutoweka na kusababisha ripoti kwamba huenda lilihusika.

Kundi hilo limeshtumiwa kwa mashambulizi ya mitandaoni mwishoni mwa mwaka uliopita ambapo michezo ya video ya Sony pamoja na Xbox ilipotea.

UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad