Mtandao wa
kijamii wa facebook ulikuwa hauingiliki katika maeneo mengi Duniani mapema leo
Januari 27,2015 kabla ya huduma zake kurudi.
Mamilioni ya
watumizi wa mtandao wa facebook walishindwa kuingia katika akaunti zao.
Wateja wake
katika mataifa mengine walishindwa hata kutumia hudumu ya Instagram.
Facebook
ilisema kuwa wahandisi wake ndio walioababisha tatizo hilo, na kukana madai kwamba
kundi moja linalotekeleza uhalifu wa mitandaoni lilihusika.
''Awali watu
wengi walikuwa hawawezi kuingia katika akaunti zao za mitandao ya facebook
pamoja na huduma ya Instagram'', msemaji wa facebook aliiambia BBC.
''Hili
halikuwa shambulizi kutoka kwa watu wengine lakini lilitokea baada ya kufanya
mabadiliko ambayo yaliathiri mpangilio wa mfumo wetu''.
Tuliharakisha
na kutatua tatizo hilo na sasa huduma zote zimerejelea asilimia 100 kama
kawaida
Mitandao
hiyo ilitoweka kwa takriban dakika 40 kabla ya kurudi.
Programu ya
mtandao unaowaunganisha wapendanao Tinder ambayo hutegemea facebook ili kutoa
huduma zake pia iliathiriwa na tataizo hilo.
Kundi moja
la uhalifu wa mitandano kwa jina Lizard Squad liliandika ujumbe kwa twitter
kuhusu hudumu hiyo kutoweka na kusababisha ripoti kwamba huenda lilihusika.
Kundi hilo
limeshtumiwa kwa mashambulizi ya mitandaoni mwishoni mwa mwaka uliopita ambapo
michezo ya video ya Sony pamoja na Xbox ilipotea.
|
No comments:
Post a Comment