NDUGU ALEX GASHAZA.
:- Huyu ni
mwanasiasa mkongwe kabisa kwenye siasa za Ngara, ukimtoa Mama Herena kwa
ukongwe hakuna mfano wake anazijua siasa za Ngara vizuri kuanzia upinzani
mpaka za chama tawala hiyo kwake ni karata ya turufu lakini pia ni kipenzi cha
watu wa pande zote mbili bughufi na bushubi kwa wanaofuatilia siasa za ngara
wananielewa vizuri lakini pia Gashaza ana sifa ya mkazi mzawa ambayo amini
usiamini ni karata yenye nguvu kubwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu 2015 kwenye
jimbo la Ngara.
Gashaza
amekua mkandarasi wa barabara na majengo kwa muda mrefu na hiyo ni taaluma yake
na hilo laweza kumjenga au kumbomoa,kumjenga kwa sababu mbili kubwa moja
limemkutanisha na watu wengi pande zote za wilaya na kujenga mahusiano na
kupanua wigo wa kufahamika.
:-Piili
ikiwa miradi aliyofanya aliitekeleza vizuri na manisha kwa kiwango na
hakudhurumu mafundi na vibarua jambo hilo kwake ni mtaji.
:-Litambomoa
likiwa mahali alipopita hakujenga mahusiano na watu na pili ikiwa hakuwapa
ujira stahiki wale waliostahili kulipwa,kama nilivyosema hapo mwanzo kuwa
Gashaza ni mkongwe kwenye siasa za Ngara, hofu yangu ni je Chama(CCM)
kinamkubali kama wananchi wanavyomkubali ..??
Nachelea
kusema ikiwa hakubaliki kwenye chama, nafasi yake ya kusimamishwa kama mgombea inabaki
shakani hata kama atashinda kwenye kura za maoni, kwa maoni yangu nikiulizwa ni
mgombea mwenye nguvu lakini asiye kuwa na milango wazi serikalini, namanisha
sio maarufu ngazi ya serikali na kichama kitaifa japo hoja hiyo sio tatizo kwa
wapiga kura wa kawaida.
NDUGU RUGUMYAMIHETO
:-Huyu ni
mtendaji mkongwe wa serikali na napata tabu kumuita mwanasiasa mkongwe kwa
sababu sheria na taratibu zetu zinawakataza watumishi wa umma kuwa wanasiasa na
kwa sababu hiyo kuwanyima fursa ya kuitwa wakongwe lakini itoshe kusema kwamba
nafasi yake ya Ukatibu ilimpa uzoefu kwani ilimkutanisha na wanasiasa wengi wa
nchi hii.
Rugumyamiheto itakua ni mara yake ya pili kugombea
kama kumbukumbu zangu zitakua sahihi, hili nalo angarabu linampa kuzijua vizuri
siasa za Ngara.
Uzoefu wake
serikalini pia ni nafasi ya dhahabu kwake kusimamishwa na chama chake kwani
uzoefu huo unaiacha milango mingi serikalini ikiwa haina kiburi cha kufunguka
mbele yake ,kikwazo kikubwa kwa Rugumyamiheto ni Je anaubavu wa kuvuka mto na kuchukua
kura ukiachilia mbali uhakika wa kuchukua kura za bugufi lakini pia utendaji
wake kama katibu mkuu unamfungulia milango ngazi ya kitaifa? je?
unamfungulia milango jimboni? anamaswali ya kujibu aliifanyia nini Ngara kwa
nafasi ya baraka aliyokuwa nayo.
Kikwazo
kingine cha wazi ni kikwazo cha ukazi kwa siasa za mwaka huu 2015 ,hilo swali
hatalikwepa na hakuna mwanasiasa yeyote anayelitaka jimbo hili mwenye ubavu wa
kuikwepa hoja ya ukazi kwani wananchi wote mijini na vijijini ukiwasikiliza wote
wanadai hawataki Wabunge wa Dar es Salaam wa Mjini wanasema wabunge wa mbezi
masaki na dodoma.
MWL.GERALD MUHILE .
:-Huyu pia
sio mkongwe au ukipenda mzoefu kwenye siasa kwa mantiki ya kwamba sheria na
taratibu za nchi haziwapi nafasi wafanyakazi wa umma kujihusisha na siasa moja
kwa moja lakini Muhile ni mtu wa watu kwa kutumia fursa ya nafasi yake ya
ualimu anabaki na mtaji mkubwa wa wapiga kura yeye amekua ,Makamu mkuu wa shule
ya Kabanga Sekondari ,Mkuu wa shule Mugoma,Mkuu wa shule Lukole na sasa Afisa
taaluma wa Idara ya Sekondari wilaya ya Ngara.
Nafasi hizi
zote zinampa kura ya turufu kwa wapiga kura wengi kama tu alizitumia
vizuri,hofu yangu ni je? chama kinamkubali ananafasi gani ndani ya chama kiwilaya na kitaifa
waweza kujiuliza kwa nini hii iwe hofu yangu kubwa,hii ni kwa sababu uzoefu
unaonesha baada ya kura za maoni chama cha Mapinduzi hufanya CHAGUO kiitikadi kwa maslahi ya chama chao na hii ni
sawa kwani ndio utaratibu waliojiwekea.
Ndugu Muhile
yeye hana kikwazo cha ukazi hii inamuongezea nafasi endapo chama kitampitisha.
|
No comments:
Post a Comment