Zitto Kabwe ni
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, mwanzoni mwa 2014 kulikuwa na story ya mgogoro
kati yake na Chama cha CHADEMA.
Magazeti
yaliyotoka siku chache zilizopita yaliripoti taarifa ya Mbunge Zitto Kabwe
kurudi tena CHADEMA, millardayo.com imepata exclusive interview na Zitto
Kabwe, kazungumzia shu hiyo.
Kuhusu
kurudi CHADEMA; “Hapana nadhani hizo ni tetesi kwa sababu sijatoa kauli
yoyote kuhusiana na hilo na moja mimi bado mwanachama wa Chadema kwa sababu
nina kesi mahakamani na kesi hiyo haijaamuliwa,bado inaendelea“– Zitto
Kabwe.
“Sijawahi
kutoka kwenye uanachama wa CHADEMA, mtu anaposema nataka kurudi Chadema hayuko
sahihi, inafahamika nilikuwa na matatizo na chama hatujaweza kuyatatua, hakuna
mazungumzo yoyote ambayo yamefanyika lakini kuna baadhi ya watu wameanza kuleta
hayo mazungumzo“– Zitto Kabwe.
|
No comments:
Post a Comment