SHERIA YETU:-Ukweli wa Polisi Kuhusu Mabomu ya Lipumba na Wenzake. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, January 29, 2015

SHERIA YETU:-Ukweli wa Polisi Kuhusu Mabomu ya Lipumba na Wenzake.

Sijui tukamate wapi baina ya kauli tofauti mbili au tatu za jeshi la polisi TZ kuhusu kadhia ya kupigwa mabomu ya machozi wafuasi wa CUF na kiongozi wao, Prof.Lipumba. Au kwa kuparangaya kiswahili niseme ‘tofauti ya kauli au kauli tofauti’. Ipi bora kwetu kuifahamu zaidi!


Awali tumeambiwa kama ifuatavyo – soma hapa chini:-Naibu kamishna wa Polisi Kanda hiyo, Simon Siro jana alisema: “Tumewakamata na tunaendelea kuwahoji… tulipewa taarifa ya maandamano hayo na viongozi wa chama na tuliwaandikia barua ya kuzuia maandamano hayo kwa kuhofia fujo kutokea.

“Sababu kubwa ya kuzuia maandamano hayo yasifanyike ni kuwa mwaka 2001 yalifanyika maandamano batili yaliyosababisha baadhi ya polisi na wananchi kufa.

Polisi tumeona, tukiruhusu maandamano haya, kuna uwezekano wa kutokea fujo kama ilivyotokea mwaka 2001.”

Alisema sababu nyingine ya kuzuia maandamano hayo ni kwamba hivi karibuni walikamatwa watu wanaojihusisha na ugaidi na kwamba kutokana na mazingira hayo polisi inazuia mikusanyiko mikubwa kwa kuhofia kutokea mambo mabaya.

Jana kauli nyengine ya polisi inasema kuwa ‘hofu kubwa ilikuwa silaha zilizoibiwa Ikwiriri, Rufiji’. Haya wpai na wapi, where is the connection! Huu ni dhahiri uwongo wa kimacho macho – na kama bunge lina ukweli na liko serious, basi wahusika laizma wawajibike maana hii kisheria ni kusema uwongo.

3. Ukipima utaona kuwa polisi limesema uwongo. Na ukisoma ‘between the lines’ utaona kuwa walipanga kufanya hujuma hii kwa visingizio tofauti – ‘ugaidi’, mara ‘silaha zilizoibiwa rufiji’, mara aliuliwa polisi 2001 Pemba — yote haya hayana mashiko. Serikali siku zote inatakiwa iwe serious, na hata kama inasema uwongo basi uwe ni uwongo wa ‘kweli’, na sio ‘uwongo’ bin uwongo bila mchuzi! au ndio ‘Wapigwe tu, na wpaigaji wapo’ — ahsante mizengo Pinda.

Source: Mzalendo
UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad