Bao pekee la mshambuliaji Danny Mrwanda limeizindua Yanga SC na kuipa
ushindi wa tano msimu huu katika mechi pekee ya Jana January 24, 2015 ya Ligi
Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) dhidi ya Polisi Moro iliyochezwa Uwanja wa
Jamhuri mjini hapa.
Mrwanda alifunga bao hilo dakika ya 42 akimalizia mpira uliotemwa na kipa
Tony Kavishe wa Polisi Moro kufuatia shuti kali la krosi ya beki wa pembeni
kulia Juma Abdul.
Hilo ni bao la tano kwa Mrwanda baada ya kufunga pia mabao manne katika
mechi saba alizokichezea kikosi cha Kocha Adolf Richard cha Polisi Moro mwanzoni
mwa msimu huu kabla ya kujiunga na Yanga SC dirisha dogo.
Mrwanda, ambaye hakufunga katika mechi mbili zilizopita ambazpo Yanga SC
ilitoka sare ya 2-2 dhidi ya Azam FC na 0-0 dhidi ya Ruvu Shooting, sasa yuko
sawa na Ame Ally Amour wa Mtibwa Sugar FC na Rashid Mandawa wa Kagera Sugar
wenye mabao matano pia.
Kwa ushindi huo, Yanga SC ambayo imeshinda mechi nyingine nne msimu huu 2014/2015
dhidi ya Tanzania Prisons, JKT Ruvu, Stand United na Mgambo ikishikwa kwa sare
na Simba SC, Azam FC na Ruvu Shooting Stars na kufungwa na wakatamiwa Mtibwa
Sugar FC na Kagera Sugar FC, imefikisha pointi 18 baada ya kucheza mechi 10.
Kikosi hicho cha Pluijm sasa kiko kimepanda hadi nafasi ya pili ya
msimamo wa VPL kikizidiwa pointi mbili na vinara Azam FC ambao pia wamecheza mechi
10 na kesho watakipiga dhidi ya Simba SC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ligi
itaendelea leo Jumapili kwa Mechi 6 na Bigi Mechi ni Uwanja wa Taifa Jijini Dar
es Salaam kati ya Mabingwa Azam FC na Simba.
Mechi
nyingine za Jumapili ni pamoja na ile ya Kagera Sugar na Ndanda FC ambayo
itachezwa Uwanja wa CCM Kirumba, Jijini Mwanza kutokana na Kaitaba Stadium kufanyiwa
ukarabati.
RATIBA.
Jumapili
Januari 25,2015.
Azam FC v
Simba
Kagera Sugar
v Ndanda FC [CCM Kirumba, Mwanza]
Stand United
v Coastal Union
Mbeya City v
Tanzania Prisons
Ruvu
Shooting v Mtibwa Sugar
JKT Ruvu v
Mgambo JKT
|
No comments:
Post a Comment