Bunge
limechachamaa na kutaka serikali ianze kuchukua hatua kali za kisheria ikiwa ni
pamoja na kuwakamata, kuwashtaki na kuwafilisi wale wote wanaohusika katika
ubadhirifu na upotevu wa fedha za serikali kutokana na kukosa uzalendo na
uwajibikaji badala ya kila mwaka bunge kupokea ripoti ya ubadhirifu
unaosababishia taifa hasara ya mabilioni ya shilingi na kwamba kujiuzulu ama
kufukuzwa kazi pekee si suluhisho ili kuwa na taifa lenye nidhamu katika
matumizi ya fedha za umma.
Bunge
limepata fursa ya kuzijadili taarifa za kamati ya bunge ya hesabu za serikali
ambayo taarifa yake inaonesha kuwa zaidi ya shilingi bilioni 100 zimekwepwa
kulipwa na makampuni mbalimbali kwa kivuli cha misamaha ya kodi na takribani
bilioni 8 nazo zikipotea baada ya mamlaka ya bandari kufanya manunuzi ya
dharura bila kibali cha mlipaji mkuu wa serikali jambo liliwafaanya baadhi ya
wabunge kugeuka mbogo.
Hata hivyo
wakati majadiliano yakiendelea kukaibuka mabishano ya kisheria dhidi ya mh
Tundu Lissu na mwanasheria mkuu wa serikali Ndg George Mcheche Masaju baada Mh
Lisu kutaka rais awawajibishe baadhi ya majaji waliohusika katika sakata la
Tegeta Escrow kwa kuwa katiba inampa mamlaka huku ndg Masaju akiliambia bunge
tume ya utumishi wa mahakama kwa mujibu wa katiba ndio inapaswa kumshauri rais
juu ya masuala ya nidhamu za majaji.
Kutokana na
kile kinachodaiwa kuwa ni kuepuka kuingilia mihimili mingine hasa mahakama
baaadhi ya wabunge wameonesha kutoridhika na hoja hiyo kutokana na wabunge
kuzuiwa kulijadili sakata la uda kutokana na taarifa za uwepo wa kesi kadha wa
kadha mahakamani zinazohusu uda baada ya mwanasheria mkuu wa serikali
kushauri kutojadiliwa bungeni kutokana na kamati ya bunge ya hesabu za serikali
za mitaa kuitaka serikali kutoa maelezo bungeni endapo ni kweli hisa za uda
zimeuzwa kwa kampuni binafsi ya simon group limited ama la.
Mara baada
ya muongozo huo mwenyekiti Mh Musa Azan Zungu akaitaka kamati uongozi ya bunge
kukutana ili kulijadili suala hilo kwa madai kuwa kuna mambo yako mahakamani na
mengine hayapo mahakamani lakini bunge linakosa fursa ya kuyajadili.
|
No comments:
Post a Comment