AFCON 2015:-Congo DR yaenda Nusu Fainali baada ya kuiadhibu Congo Brazaville. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, January 31, 2015

AFCON 2015:-Congo DR yaenda Nusu Fainali baada ya kuiadhibu Congo Brazaville.

DR Congo ilitoka nyuma na kuishinda Congo kwa mabao 4-2 huko Estadio de Bata Mjini Bata Nchini Equatorial Guinea na kutinga Nusu Fainali ya AFCON 2015.

Robo Fainali za AFCON 2015, Kombe la Mataifa ya Afrika,iliwashuhudia Congo DR iliyotoka nyuma 2-0 na kuishinda Congo katika mechi iliokuwa na kasi na mchezo mzuri kutoka pande zote mbili.

Ferebory Dore alifunga krosi safi huku Thievy Bifouma akifunga pia na kuwa mabao 2-0.

Katika dakika ya 16 Diermerci Mbokani alifunga bao la kwanza ,kabla ya Bolika kufunga bao la pili naye Joel Kimuaki akafunga bao la tatu.

Wachezaji wa Congo wakisherehekea ushindi.

Mbokani aliwazunguka tena mabeki wa Congo na kufunga bao la nne na la ushindi katika shambulizi la ghafla.

Baadae Usiku huu ipo Mechi nyingine ya Robo Fainali kati ya Wenyeji Equatorial Guinea na Tunisia.

Hapo Kesho Februari 01,2015,Robo Fainali itakamilika kwa Ghana na Guinea kucheza huko Estadio de Mongomo Mjini Mongomo na kufuatiwa na Ivory Coast na Algeria huko Nuevo Estadio de Malabo Mjini Malabo.

Washindi wa Mechi hizo 4 watatinga Nusu Fainali.


Jumapili Februari 1,2015.

1900 Ghana v Guinea [Estadio de Mongomo] 
  
2200 Ivory Coast v Algeria [Nuevo Estadio de Malabo]  
      
NUSU FAINALI

Jumatano Februari 4,2015.

2200 Congo DR v Ivory Coast/Algeria [Estadio de Bata]=NF1   
     
Alhamisi Februari 5,2015.

2200 Tunisia/Equatorial Guinea v Ghana/Guinea [Nuevo Estadio de Malabo]=NF2

MSHINDI WA 3

Jumamosi Februari 7,2015.

2100 Aliefungwa NF1 v Aliefungwa NF2 [Nuevo Estadio de Malabo]

FAINALI

Jumapili Februari 8,2015.

2200 Mshindi NF1 v Mshindi NF2 [Estadio de Bata]    



UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad