Timu ya Taifa ya Guinea imeshinda kamari iliyopigwa kupata timu ya pili
ya kundi D inayofuzu robo fainali ya kombe la Mataifa ya Africa, Afcon 2015 na
sasa itacheza na Ghana katika hatua hiyo.
Sheria ya CAF kipengele cha 74 kimetumika kuamua mshindi baina ya Mali na
Guinea ambao walimaliza wakifanana kwa kila kitu.
Sheria hiyo pia inatumika na shirikisho la soka Duniani FIFA.
Timu
zikifungana kila kitu basi hufanywa Bahati Nasibu ili kupata Mshindi na hii ni
mara ya kwanza kwa Mshindi kupatikana kwa njia hii kwenye Mashindano haya tangu
1988 wakati Algeria iliposhinda Tombola hiyo na kuibwaga Ivory Coast.
Mbele ya
Kamati ya Matayarisho ya CAF, Rais wa Mali, Boubacar Diarra, ndio alikuwa wa
kwanza kutoa Kimpira toka kwenye Chungu chenye Jina la Nchi yake na hivyo
kuthibitisha wamemaliza Kundi D wakiwa Nafasi ya 3 na akaja Amara Dabo,
Mkurugenzi wa Fedha wa Wizara ya Fedha ya Guinea, ambae aliokota Mpira wa Pili
uliobakia ambao ulithibitisha Guinea wamemaliza Nafasi ya Pili nyuma ya
Washindi wa Kundi D, Ivory Coast na hivyo kusonga Robo Fainali.
AFCON 2015 RATIBA.
**Saa za Bongo
ROBO FAINALI
Jumamosi Januari 31,2015.
1900 Congo v
Congo DR Kundi B [Estadio de Bata]=RF1
2200 Tunisia
v Equatorial Guinea [Estadio de Bata]=RF2
Jumapili Februari 1,2015.
1900 Ghana v
Guinea [Estadio de Mongomo]=RF3
2200 Ivory
Coast v Algeria [Nuevo Estadio de Malabo]=RF4
NUSU FAINALI
Jumatano Februari 4,2015.
2200 RF 1 v
RF4 [Estadio de Bata]=NF1
Alhamisi Februari 5,2015.
2200 RF2 v
RF3 [Nuevo Estadio de Malabo]=NF2
MSHINDI WA 3
Jumamosi Februari 7,2015.
2100
Aliefungwa NF1 v Aliefungwa NF2 [Nuevo Estadio de Malabo]
FAINALI
Jumapili Februari 8,2015.
2200 Mshindi
NF1 v Mshindi NF2 [Estadio de Bata]
UNGANANASI KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Friday, January 30, 2015
Home
MICHEZO
AFCON 2015:-Baada ya Guinea kupita kwa kamari sasa hii ndio Ratiba ya Robo Fainali kuwavaa Ghana.
AFCON 2015:-Baada ya Guinea kupita kwa kamari sasa hii ndio Ratiba ya Robo Fainali kuwavaa Ghana.
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment