MWANANCHI
Mgombea
Uenyekiti kupitia Chama cha CCM Mtaa wa Swea kata ya Mkolani Mwanza Pius Mihayo
amefariki dunia gafla akiwa mtaani kwake muda mfupi baada ya kupiga kura.
Msimamizi wa
uchagyzihuo Halifa Hida alisema mgombea huyo alifariki dunia gafla akiwa kwenye
mtaa wake wa Swea na chanzo cha kifo chake hakijajulikana.
“Sasa kwa
mujibu wa taratibu za uchaguzi,tutatangaza matokeo ya wajumbe na nafasi za
wagombea wa vitimaalum,nafasi ya uenyekiti haitatangazwa hadi taratibu nyingine
za uchaguzi zitakapoandaliwa”alisema Hida.
Mkoani
Arushamsongamano wa wapigakura katika kituo chaMbauda kata ya Sombetini
unadaiwa kusababisha kifo cha mtu aliyetambulika kwa jina la Suleiman Bakari.
Tukio hilo
lilitokea saa 3 asubuhi katika kituo hicho ambacho kilikua kimefurika watu
ambapomtu huyo alianguka gafla baadaya kukosa hewa akiwa kwenye mstari wa
kupigakura.
NIPASHE
Uchaguzi wa
Serikali za mitaa,vijiji na vitongoji ulifanyika nchini kote jana huku
ukitawaliwa na kasoro na vurugu kubwya zilizosababishapolisi kutumia
risasi za moto na baadhi ya wapigakura kuchapana makonde jijini Dar es salaam.
Vurugu hizo
zilitokana na uchaguzi huo kugubikwa na kasoro nyingi na hivyo kusababisha
baadhi ya vituo kulazimika kuahirisha uchaguzi huo hadi wiki ijayo.
Baadhiya
kasoro zilizoibuka zilitokana na baadhi yavituo kuchanganya majina ya
wagombea,kuchelewa kuanza kwa uchaguzi,kukosekana kwa vifaa vya kupigia kura
pamoja na baadhi ya wagombea kuwahujumu wengine.
Uchaguzi huo
ulipangwa kuanza saa2 asubuhi lakini maeneo mengi ulichelewa kuanza kutokana na
vifaa kuchelewa kufika vituoni.
Katika kituo
cha Kimara bucha kulitokea vurugu kubwa baada ya mawakala kugombea kuwasaidia
wapigakura kuweka alama ya vyema kwa wagombea na baadhi ya watu kutakakurudia
kup[iga kura hali iliyosababisha msimamizi wa kituo hicho kupigwa na wapigakura
kutokanana na kukerwa na kitendo cha baadhi yawatu kurudia kupiga kura.
NIPASHE
Naibu Waziri
wa Nishati na Madini Stephen Masele ambaye pia ni Mbunge wa Shinyanga mjini
amevamiwa na kundi la vibaka wakati akienda Zahanati kupatiwa matibabu na kisha
kuporwa vitu mbalimbali mjini Shinyanga.
Masele
alisema tukio hilo lilitokea juzi saa4 usiku wakati akienda kupatiwa matibabu
ya matatizo ya koo katika Zahanati ya Bakwata na gafla alivamiwa na kundi
la watu wapatao 30 na kumpora mali zake.
Alisema
akiwa na Naibu Katibu mkuu CCM Zanzibar,Vuai Aly wakipata chakula cha usiku
hotelini gafla alijisikia vibaya na kuamua kwenda kwenye Zahanati hiyo kupatiwa
matibabu na ndipo alipata mkasa huo wakati akiwa njiani.
Masele
alikanusha tuhuma alizozushiwa na wananchi kuwa kuporwa huko kunatokana na yeye
kugawa rushwa kwa wananchi wakati wa kampeni Serikali za mitaa ili wananchi
wawachague wagombea wa CCM.
MTANZANIA
Katibu wa
CCM kata ya Narungombe Lindi Mohamed Pilipili amevamiwa na kupigwa hadi kuzimia
na mabaunsa kwa madai ya kufanya kampeni ya nyumba kwa nyumba usiku.
Tukio hilo
lilitokea juzi usiku katika kitongoji cha Chikwale baada ya kundi la mabaunsa
kumvamia na kumpiga Katibu huyo pamoja na Mwenyekiti wa CCM wa kata hiyo
Seleman Lukuche.
Akizungumzia
tukio hilo Lukeche alisema ilikua saa 3 usiku wakitoka Ruangwa kupeleka taarifa
za mwenendo wa uchaguzi pamoja na majina ya mawakala wa CCM ndipo walipovamiwa
na kundi hilo la mabaunsa10waliodai wao wanadhibiti .vitendo vya ryushwa ambao
walianza kuwapiga bila kutaka maelezo.
Katika tukio
jingine mgombea wa nafasi ya uenyekiti kata ya Mkwajuni amepigwa na watu
wanaodaiwa wafuasi wa CUF kwa madai kuwa alikwenda kwenye eneo la Mjimwema
kupanga mikakati ya kuiba kura.
UHURU
Muda wowote
kuanzia sasa Rais Jakaya Kikwete atatoa na kutangaza uamuzi wake kuhusiana na
baadhi ya watendaji wakiwemo Mawaziri kuhusishwa katika kashfa ya wizi wa fedha
za Tegeta Escrow.
Wiki
iliyopita Rais alipokea na kupiia ripoti iliyowasilishwa kwake,nyaraka na
ushauri uliotolewa katika maazimio ya Bunge kuhusu akaunti ya Tegeta Escrow.
Kikwete
ambaye alianza kazi Desemba 8 mwaka huu baada ya mapumziko kutokana na
kufanyiwa upasuaji alisema atatoa uamuzi wake ndani ya wiki hii.
Alisema
atatolea maamuzi mambo ambayo yanamuhusu yeye moja kwa moja na yale yanayohusu
Serikali atatolea uamuzi na maelekezo ya namna ya kuyashughulikia.
Bunge
lilitoa maazimio mbalimbali kwa Serikali ikiwemo kuitaka mamlaka ya uteuzi
kuwawajibisha ikiwani pamoja na kuwavua nyadhifa zao Waziri wa Nishatina
Madini,Mwanasheria mkuu,Waziri wa nyumba na maendeleo ya makazi,Katibu mkuu wa
Wizara ya Nishati na madini na wengineo.
HABARILEO
Kundi la
watu wanaodhaniwa kuwa majambazi wamevamia na kupora fedha na vitu mbalimbali
ndani ya kanisa Katoliki la Kilema jimbo la Moshi vijijini Mkoani Kilimanjaro.
Tukio hilo
lilitokea usiku wa kuakia jana ambapo watu hao wakiwa na vifaa maalum vya
kuvunja milango,walivunja langokuu la kanisa hilo na kuvunja sanduku la sadaka
na kupora vifaa vya kufanyia ibada.
Padri wa
Parokia ya Kilema DamianTemere alisema vitu vilivyoibwa ni pamoja na vifaa
vitakatifu vinavyotumika katika sikukuu ya Ekaristi na majambazi hayo yalivunja
kasha la kuhifadhia sadaka na kupora fedha zilizokuwemo ambazo hazikujulikana
thamani yake.
Alisema pia
waliiba vifaa vya kunywea divai na kumunio ambavyo nivya dhahabu vyenye thamani
ya mamilioni ya fedha huku wakiacha vile vya shaba.
Alisema
baadhi ya vifaa hivyo vilinunuliwa na wamisionari wa kwanza na vilikua na
thamani kubwa kwa kanisa hilo kwa kuwa niliwakilisha imani katika parokia hiyo
na kanda nzima ya Kaskazini.
MWANANCHI
Shirika la
usafiri wa anga la China Avic International liko kwenye mazungumzo na Shirika
la ndege la hapa nchini ATCL ili kuliwezesha Shirika hilo la Tanzania kufanya
kazi kwa ufanisi.
Avic
inayomilikiwa na Serikali ya China imesema mkakati wake wa kwanza ni kutoa
ndege kwa ATCL ili kuboresha huduma zake,kufanya kazi na kujiendesha kama
ilivyo kwa mashirikayandege ulimwenguni.
Naibu Katibu
mkuu wa Wizara ya UchukuziMonica Mwamunyange alisema kituo hicho kimeanzishwa
baada ya makubaliano ya nchi mbili yaliyofanyika China mwezi Oktoba mwaka huu
wakati Kikwete alipotembelea nchi hiyo.
“Tuliangalia
suala la kuunganisha nguvu kati ya ATCL na Avic International na tayari wenzetu
wa China wameamua kuanzisha kituo hiki”alisema Mwamunyange.
UNGANANASI
KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
No comments:
Post a Comment